EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Friday, October 18, 2013

RAISI PAUL KAGAME AMESEMA MAREKANI HAIMTISHI NA HATUA ZAKE ZA KUSITISHA MSAADA KWA NCHI YAKE



Rais wa Rwanda, Paul Kagame amesema nchi yake haitishwi na hatua iliyochukuliwa na serikali ya Marekani, kusitisha msaada wake wa kijeshi kwa nchi hiyo, kwa kile inachodai Rwanda inawafadhili waasi wa M23 wanaopigana na serikali mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC.
 
Raisi wa Rwanda Paul Kagame
Rais Kagame amesema anashangazwa na hatua ya Marekani kuihukumu nchi hiyo kwa makosa ambayo Rwanda haihusiki kwa lolote wala haifadhili kundi lolote la waasi nchini DRC na kuongeza kuwa kufanya hivyo ni kutoitendea haki Rwanda. Rais Kagame amesema kamwe Rwanda haijawahi kuhusisha watoto wadogo kwenye jeshi lake wala kuunga mkono kutumikishwa kwa watoto wadogo kama wanajeshi kwenye kundi la M23. Serikali ya Marekani ilitangaza majuma kadhaa yaliopita kusitisha msaada wake wa kijeshi kwa serikali ya Rais Kagame kufuatia hatuwa hiyo inayotajwa ya kuwafadhili waasi wa kundi la M23 wanaopambana na serikali ya Rais Joseph Kabila.

No comments:

Post a Comment