EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, May 23, 2013

KAKA, DADA WANASWA WAKIDUU COCO BEACH,

KAKA, DADA WANASWA WAKIDUU COCO BEACH, MCHEZO MZIMA ULIKUA HIVI!


UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Firauni. Usemi huu unakamilishwa na tukio la kunaswa kwa vijana wawili wenye undugu wa damu wakifanya mapenzi ‘wakiduu’ kando ya Ufukwe wa Bahari ya Hindi!
Imefahamika kwamba vijana  hao, kaka na dada (majina tunayo)  wamenaswa ‘wakiduu’ katika mapango yaliyopo kando ya Ufukwe wa Coco, Oysterbay jijini Dar es Salaam.

TUKIO ZIMA
Tukio zima lilitokea mchana kweupe wa saa 9 na kudhihirisha habari za mara kwa mara zinazoeleza kwamba Ufukwe wa Coco umekuwa ukitumika kwa ufuska usiku na mchana.
Risasi Mchanganyiko lilinasa tukio hilo kwa kutumia mitambo maaalum iliyoelekezwa kando ya bahari.
Wawili hao walinaswa tangu walipokuwa wakiingia katika ufukwe huo na kuwafuatilia nyendo zao, hatua kwa hatua.
DEMU ALIKUWA AKIZINGUA
Haikufahamika mara moja kama wawili hao walikuwa na makubaliano ya kwenda kuduu katika ufukwe huo au la, lakini kwa mbali ilionekana kama vile dada mtu alikuwa akizingua kwenda kutenda dhambi hiyo.
Picha za video zilizonaswa, zinamuonesha dada huyo akionekana kutoa upinzani pale alipokuwa akishikwashikwa na kaka yake.
Alionekana kama vile hakuwa tayari kwa mchezo huo.
Hata hivyo, kaka mtu anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 23-26 alikuwa akilazimisha kitu fulani ambacho kilionekana dhahiri kupitia kamera zetu.
Ni kama vile hawakuwa na makubaliano na kile walichokuwa wakienda kukifanya.
Mara kadhaa dada huyo alionekana kumkwepa kaka yake na alikuwa akijiondoa karibu yake pale alipomlazimisha kutaka kumfanyia kitu kisichokuwa cha kawaida.

KAMERA ZAELEKEZA KWAO
Kamera za Risasi Mchanganyiko ziliwafuatilia wawili hao kwa kuwa walionekana kuwa na kitu ‘spesho’.
WAINGIA MAPANGONI
Mpaka wanazama katika mapango yaliyopo kando ya ufukwe huo wa Coco, kamera zilikuwa zikiendelea kuwachukua hadi walipozama ndani kabisa ya mapango hayo.
WANASWA LIVE
Walipozama ndani ya mapango hayo, ghafla walitokea askari ambao nao walikuwa wakifuatilia nyendo za wawili hao.
Askari hao wa Kituo cha Oysterbay, wakiongozwa na kamanda wa oparesheni maalumu katika Wilaya ya Kinondoni, Kamanda Swai walifuatilia kwa umakini tukio hilo.
WANASWA
Wakiwa chini ya mapango, kaka na dada waliondoa ‘viwalo’ vilivyokuwa maungoni mwao na kuanza kuduu kama vile walikuwa katika ufukwe unaoruhusiwa kufanya vitendo hivyo.
WAKUTWA WATUPU
Kabla askari hawajawavamia, waliwashuhudia wawili hao wakiwa katika kilele cha sterehe yao huku dada mtu akionesha kutoa ushirikiano kwa shingo upande.
Ghafla, askari waliwavamia na kuwatibulia starehe yao kisha kuwatia mbaroni.

No comments:

Post a Comment