Jaji Buxton Chipeta.
Habari
zilizotufikia hivi punde zinasema kwamba Jaji mstaafu wa Mahakama Kuu
Tanzania, Buxton Chipeta amefariki dunia muda mfupi uliopita.
Kwa
mujibu wa mmoja wa wanafamilia, Jaji Chipeta alikuwa akisumbuliwa na
maradhi ya kisukari ambapo ilifikia wakati akalazimika kukatwa vidole
kadhaa vya miguuni.
Enzi za uhai wake, Jaji Chipeta aliweza
kujijengea heshima katika kazi yake na kufikia kuwa mmoja wa majaji
wanaoheshimika mno hapa nchini.
Pia Jaji Chipeta aliwahi kuwa miongoni mwa majaji wa Tume ya kurekebisha Sheria yeye akiongoza kanda ya Dar es Salaam.
Mpekuzi inaungana na familia ya...
WITO WA KUPINGA KODI YA LAINI YA SIMU KILA MWEZI KUFUATIA MABADILIKO YA SHERIA YA KODI 2013
Sisi
wananchi hatujashirikishwa kupitia mjadala wa Bunge kuhusu kodi hii
kwani Waziri wa fedha hakusoma hiki kipengele wakati wa hotuba yake na
tulikosa taarifa mpaka baada ya kupitishwa kwa sheria ya kodi hii.
Kodi hii inamkandamiza mtanzania wa hali ya kawaida na wa hali ya chini
ambao ni 67% ya wananchi wanaoishi chini ya kipato cha dola 1.25 (shs
2,000) kwa siku. Takwimu zinaonyesha kuwa kati wa wamiliki wa laini za
simu milioni 22, milioni 8 wanatumia chini ya shilingi 1,000 kwa mwezi.
Serikali inaweza punguza matumizi yake mengineyo (safari, posho,
semina, manunuzi ya magari na kudhibiti ufisadi) hivyo kufidia pengo...
No comments:
Post a Comment