Mwanamke mmoja Sumayi Girandi mkazi wa kijiji cha Kunzugu
wilayani Bunda amepoteza vidole vitatu vya mkono wa kulia na kiganja cha
mkono wa kushoto kukatwa baada kushambuliwa kwa mapanga na watu
wasiojulikana kisa kikidaiwa kuwa kutaka kunyang’anywa mali zake.
Uhodari
wa mama huyo wa kutafuta mafanikio ya familia yake hasa baada ya
kutengana na mume wake umeishia hapo baada ya watu wasiojulikana
kumvamia nyumbani kwake na kumshambulia kwa mapanga na kisha
wakamkata kiganja cha mkono wa kushoto na kuanguka.
Kwa
sasa Sumayi Girandi anatibiwa katika Hospitali teule ya wilaya.
Vitendo vya kujeruhi na kuua wanawake...
BONDIA AUAWA KWA KUCHOMWA KISU......ALIKUWA AKIAMULIA UGOMVI KABLA YA KISANGA KUMGEUKIA
BONDIA maarufu Ramadhani Idd ‘Mashudu’ ameuawa kwa kuchomwa visu mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Tukio
hilo lililowaacha midomo wazi wakazi wa Mabibo Loyola, Wilaya ya
Kinondoni jijini Dar es Salaam lilitokea saa sita usiku Julai 4, mwaka
huu.
Imedaiwa kuwa, marehemu aliwakuta Jack Mchaki na mtu mwingine wakigombana, alipowaamulia wakamgeuzia kibao na kumchoma visu.
Waandishi
wetu walifika eneo la tukio na kukutana na mashuhuda waliozungumza kwa
sharti la kutoandika majina yao , mmoja alidai marehemu alikuwa
anaangalia kanda za filamu katika banda moja maeneo hayo ghafla alifika
Jack aliyelewa na kuanza kufanya fujo.
Shuhuda...
GIZA LATANDA KWA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO....MSIMU WA MASOMO UMEANZA HUKU "SELECTION" ZIKIWA BADO
Matokeo mabaya ya kidato cha nne ya mwaka 2012, yameendelea
kuitikisa sekta ya elimu nchini baada ya shule kufunguliwa jana bila
kutangazwa kwa waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka huu.
Kwa kawaida, wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga na
kidato cha tano na vyuo vya ualimu, hutangazwa mapema ili kutoa fursa
kwa wanafunzi na shule husika kufanya maandalizi ya mahitaji.
Lakini tofauti na ilivyozoeleka, wanafunzi wa
kidato cha sita walianza masomo yao jana huku wale wanaotarajiwa
kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ualimu wakiwa hawajatangazwa.
...
MBUNGE WA DODOMA MJINI AWATEMBELEA WAHANGA WAMLIPUKO WA PETROL KATIKA HOSPITAL YA MKOA WA DODOMA
Mbunge wa Dodoma mjini Mh
Dr David Mallole, alipoenda kuwatembelea wahanga wa mlipuko wa Petrol
katika hospital ya mkoa wa Dodoma,General Hospital na kutoa pole kwa
wagonjwa waliopatwa na janga hilo kwa kuwapatia pole pamoja na msaada wa
pesa ya dawa kwa kila mmoja
Mtoto huyu ni mwanafunzi wa kidato cha tatu Shabani p. Shaban .Alikutana
na janga hili baada ya kwenda kwa fundi kuchukua nguo zake za
shule ambapo ni eneo jirani na mlipuko huo ulipotokea. Mh Mbunge David
Mallole ameahidi kumlipia ada yake ya shule:
Credit: Bossngasa blog...
HUDUMA YA TRENI LA JIJI KESHO HAIPO....KICHWA KIMOJA NI KIBOVU
Uongozi wa Kampuni ya
Reli Tanzania –TRL unasikitika kuwataarifu wananchi na wakazi wa jiji
kwa jumla kuwa huduma ya treni ya jiji haitokuwepo kwa muda wa siku 2
kuanzia leo Julai 8, 2013 kutokana na hitilafu kubwa katika kichwa
kimojawapo cha treni hiyo.Uamuzi huo unatokana na sababu za kiufundi
unaosimamia uendeshaji wa huduma hiyo jijini.
Kwa
utaratibu huduma hii huendeshwa kwa kutumia vichwa vya treni vitatu
ambapo viwili uhudumia moja kwa moja na cha tatu huwa cha akiba .
Kuanzia siku ya Jumamosi ambapo huduma haikuwepo, kichwa cha tatu
kiligundlika kuhitaji matengenezo makubwa na kupelekwa katika karakana
yetu ya Morogoro.
Kutokana
na utaratibu tulioainisha hapo awali kukosekana kichwa cha dharura
’standby’ kunalazimisha tusitishe huduma kwa muda. Hata...
SABABU TANO ZILIZOWAFANYA CHADEMA WAGOME KUSHIRIKI "KONGAMANO LA AMANI" LINALOANZA KESHO
Ndugu waandishi wa habari,Tumewaiteni hapa mchana huu kwa
dharula, kutokana na kujitokeza kwa jambo moja muhimu sana katika
mustakabali wa chama chetu na taifa kwa ujumla. Jambo lenyewe ni hili:Kwa muda
wa siku mbili, kuanzia kesho– tarehe 9 Julai 2013 hadi 10 Julai –
kutakuwa na “KONGAMANO LA AMANI” lililoitishwa na Kituo cha Demokrasia
Tanzania – Tanzania Center For Democracy (TCD).Kongamano hilo
linatajadili na kutafakari Amani ya Taifa, litafanyika kwenye hoteli ya
White Sands ya jijini Dar es Salaam. Litafuguliwa na Mwenyekiti wa TCD,
Mbunge wa kuteuliwa na Rais, Mheshimiwa James Mbatia na litafungwa na
Rais Jakaya Kikwete.Baadhi...
UWOYA AAMBULIA MATUSI BAADA YA KUMFANANISHA DIAMOND NA MICHAEL JACKSON
Mwigizaji wa filamu za Kibongo, Irene Pancras Uwoya, amelowa mvua ya
matusi baada ya kumfananisha mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’
na aliyekuwa mwanamuziki mkubwa duniani, marehemu Michael Jackson.
Wikiendi iliyopita, Uwoya aliandika kwenye ukurasa wake katika mtandao
wa Instagram kuwa msanii huyo anayefanya vizuri katika Bongo Fleva ndiye
staa atakayemrithi mkali huyo wa Pop, maandishi ambayo yalizua matusi
hayo ya nguoni.
Baadhi ya mashabiki wa mastaa hao walitoa maoni kuwa
jambo hilo ni sawa na kufananisha vitu ambavyo havina uwiano hasa
ukizingatia Michael Jackson alishafariki dunia Juni 25, 2009.
“Sasa...
"PREZZO ANAYAJUA MAPENZI.....HATA AKINIUTHI SITAHESABU MAKOSA YAKE"....DIVA WA CLOUDS FM
Muda mfupi
uliopita mtangazaji wa ‘Ala za Roho’ ya Clouds FM Diva Loveness Love
ambaye sasa anatumia “divathebawse” katika akaunti yake ya Instagram,
ameweka picha mpya akiwa na Rapcellency Jackson makini aka Prezzo kutoka
Kenya waliyopiga jana (July 7).
Picha hiyo ambayo inawaonesha wawili hao wakiwa “0 distance” ilikuwa na
caption inayosomeka hivi,
“Nothing Than Happiness… Prez is such a Nice guy. Hata Akiniudhi
Sihesabu makosa yake. May you Live Long Pleaseeee……… Good hearted, My
hero, My Mentor… A Person I can count to when I need to be happy… No one
is Perfect yes but I love his flaws and All…. Bless you always’ . I
Pray you...
UGONJWA WA KIPINDUPINDU WALITIKISA JIJI LA MBEYA...MIKUSANYIKO YAPIGWA MARUFUKU
UGONJWA wa kipindupindu, umeingia katika wilaya ya Kyela na kuua watu wawili na 39 wakiwa wamelazwa.Taarifa
zinasema ugonjwa huo umeibuka wilayani humo wiki iliyopita ukisadikika
kuanzia katika Kijiji cha Ngonga na kisha kusambaa hadi Kilwa.Kutokana
na hofu ya kupata maambukizi kwa wananchi wengine, serikali imepiga
marufuku mikusanyiko ikiwemo ya harusi, kipaimara, ngoma, michezo na
sikukuu inayosherehekewa kila mwaka ya wakulima. ...
ANGALIZO:MAFUTA YA UBUYU YANA TINDIKALI INAYOSABABISHA SARATANI
Baada ya kuonya wananchi
wanaotumia dawa za tiba mbadala ambazo hazijathibitishwa, Mamlaka ya
Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), sasa inawataka wananchi kuacha kutumia
mafuta ya ubuyu kwa kunywa kama dawa.
Akizungumza
juzi katika Maonesho ya 37 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam,
msemaji wa TFDA, Gaudensia Simwanza, alisema Mamlaka hiyo ilipima na
kubaini mafuta hayo yana tindikali ya mafuta.
Alifafanua katika
maonesho hayo maarufu kama Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya
Mwalimu J.K. Nyerere, kwamba mafuta hayo hayafai kuliwa na binadamu na
anayekunywa kwa wingi, yuko hatarini kupata saratani za aina tofauti
tofauti....
No comments:
Post a Comment