MAGWIJI wa Manchester United, Paul Scholes, Bryan Robson ana Edwin van der Sar ni baadhi ya wachezaji wa zamani wa Mashetani hao Wekundu watakaocheza mechi ya hisani dhidi ya nyota wenzao wa kitambo wa Bayern Munich Jumamosi.
Mechi hiyo itakayofanyika Uwanja wa
Allianz Arena, itashuhudiwa mabingwa wa sasa wa Bundesliga wakimenyana na
wakali wanzao wa enzi hizo wa United.
Timu hizo mbili zilikutana katika
mechi kadhaa enzi zao, lakini zaidi mpambano ambao bado upo kwenye
kumbukumbu za wengi ni wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 1999, ambayo
United ilishinda katika msimu waliotwaa mataji matatu.
Paul Breitner - aliyeiongoza
Ujerumani Magharibi kutwaa Kombe la Dunia mwaka 1974 atakuwa Nahodha wa Bayern
Munich ambayo itakuwa pia na wakali kama Marc van Bommel na kiungo wa
zamani wa United, Owen Hargreaves.
Kikosi cha United pia kitahusisha
wakali wa zamani kama Dwight Yorke, Andy Cole, Ronny Johnsen na Quinton
Fortune. Mwenyekiti wa Bayern, Karl-Heinz Rummenigge amesema: "Nina
uhakika litakuwa tukio moja maalum sana,".
Fedha zitakazopatikana katakana
na mauzo ya tiketi zitakwenda katika mfuko wa kituo cha watoto cha Allianz.
No comments:
Post a Comment