HABARI
za motomoto kutoka vyanzo vya uhakika, zinasema kuwa staa wa kike
anayekuja juu kwa sasa katika tasnia ya filamu Bongo, Yobnesh Yusuph
‘Batuli’ ameitikisa ndoa ya mwigizaji mwenzake, Nice Mohammed ‘Mtunis’
kwa madai ya kutoka naye kimapenzi.
Chanzo chetu, kwa sharti la kutochorwa jina lake gazetini kilifunguka
kuwa ishu ya wawili hao kuwa wapenzi siyo siri, kwani mara kadhaa
wamekuwa wakijiachia sehemu mbalimbali, huku mke wa Mtunis
akinyetishiwa, jambo lililosababisha migongano ndani ya ndoa hiyo.
“Mmechelewa kweli kujua! Leo ndiyo mnauliza kuhusu Mtunis na Batuli?
Hao ni wapenzi na penzi lao limenoga kwelikweli sasa hivi. Imefikia
hatua Mtunis na mkewe hawana maelewano mazuri. Nyumba ni kama
inayumbishwa na Batuli lakini Mtunis hataki kumwacha Batuli,” kilipasha
chanzo hicho.
MTUNIS KIKAANGONI
Kama ada, Risasi Mchanganyiko
lina desturi ya kupata mzani wa habari kabla ya kuirusha, ndivyo
ilivyofanyika kwa Mtunis ambaye aliposomewa mashitaka yake alipovutiwa
waya, alikanusha vikali akidai ndoa yake ina amani na hana uhusiano na
Batuli.
“Kwanza nani amekuambia kuwa mimi natoka na
Batuli? Yule ana mtu wake
na mimi nina ndoa yangu. Sikia kaka, katika kipindi ambacho ndoa yangu
ina amani ni hiki, sitaki kabisa haya mambo. Mtakuja kusababisha Batuli
agombane na mumewe kisa mimi,” alisema Mtunis kwa sauti ya juu.
BOFYA HAPA KUMSIKIA BATULI
Batuli alipopatikana
kwa njia ya simu, alikuwa msikivu muda wote alipoelezwa kuhusu madai
hayo, mwishoni akajibu kwa mtindo wa kuuliza: “Kwanza nikuulize, Mtunis
ni Muislam au Mkristo?”
Mwandishi wetu alipomjibu kuwa ni Muislam, akaendelea: “Sasa kipi cha
ajabu hapo? Kwa imani yake ya Kiislam, ana ruhusa ya kuoa wake hadi
wanne. Halafu kuna wakati nilishaishi naye miaka si chini ya minne, kwa
hiyo sioni ajabu hapo. Hata kama ikitokea tena hakuna tatizo.
KUITIKISA NDOA YA MTUNIS
“Achana na watu bwana,
acha tu watu waongee. Lakini ninachosema hakuna cha ajabu hapo. Maisha
yanaruhusu, yaani kisheria hata Mungu anaruhusu - siyo ajabu. Siwezi
kuzungumza zaidi maana nimesafiri nipo kwenye harusi, dada yangu
anaolewa.”
CHANZO>>>>GLOBAL PUBLISHERS
No comments:
Post a Comment