EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Friday, February 14, 2014

KESI YA MWANGOSI WAANDISHI WA HABARI WAISHITAKI POLISI IRINGA KWA KUMFICHA MTUHUMIWA



NA: MATHIAS KANAL........IRINGA
Mapema hii leo askari Pacificus Cleophace Simon mwenye No G.2573 mtuhumiwa wa kesi ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha channel ten mkoani Iringa Daud Mwangosi amefikishwa mahakamani kusomewa shitaka la kesi hiyo kwa mara ya kwanza
Cleophace amesomewa shitaka hilo linalomkabili kutokana na mauaji ya mwandishi huyo wa habari yaliyotokea kijiji cha Nyololo Wilayani Mufindi Mkoa wa Iringa wakati wa mkutanao mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema uliotarajiwa kufanyika septemba 2, 2012 na kuhutubiwa na katibu mkuu wa chama hicho Dkt Wilbroad Slaa
Hata hivyo serikali iliikiandikia barua  chama cha demokrasia na maendeleo chadema ya kuwataka kusitisha mkutano kwa siku hiyo kwa sababu siku hiyo hiyo sensa ya watu na makazi ilianza na badala yake ilikitaka chama hicho kusubiri hadi sensa itakapomalizika septemba 8, 2012
Chama cha chama cha demokrasia na maendeleo chadema hakikubaliana na maagizo hayo ya serikali kwa kuwa tayari kilikuwa na barua ya kuruhusiwa kufanya mkutano huo hivyo kupelekea kuwa na mvutano kati ya jeshi la polisi na wafuwasi wa chama hicho hivyo kupelekea polisi kupiga mabomu ya machozi kwa ajili ya kuwatawanya wafuasi hao waliojitokeza kwenye mkutano huo.
Baada ya uchunguzi wa chanzo cha kifo hicho mkemia mkuu alitoa uthibitisho kuwa kilichomuua Mwangosi ilikuwa ni kemikali aaina ya NItrate na Cloride zilizokutwa zimebakia katika mwili wa Marehemu Mwangosi.
Wakati huo huo kesi ikiwa inaendelea mapema hii leo, askari wa jeshi la polisi alevaa nguo za kiraia jina halijafahamika simu yake iliita mahakamani na kutoka nje kwa ajili ya kuipokea kitendo ambacho ni kinyume na utaratibu wa uendeshaji wa mahakama lakini hakuchukuliwa hatua yoyote.
Sambamba na hayo Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa Bw Frank Leonard ambaye ni mwandishi wa gazeti la habari leo na mmiliki wa TOVUTI ya BONGO LEANKS alikamatwa na askari na kutolewa nje ya mahakama kwa kuwa alishika simu wakati mahakama inaendelea hivyo kuhisiwa alikuwa anapiga picha.
Leonard alifikishwa kituo kikuu cha polisi kwa ajili ya kujibu tuhuma hizo huku waandishi wote walihudhuuria mahakamani hapo wakiwa nje ya kituo hicho kusubiri hatma ya kesi hiyo.
Haikuchukua hata dakika 2 Leonard akaachiwa huru kwa kuwa jeshi la polisi liijichukulia sheria mkononi wakati jambo lolote la kimahakama linapaswa kuamuliwa na kjaji anayeendesha kesi hiyo.
Aidha jaji mfawidhi wa mahakama ya Iringa Bi Mary Shangai ameahirisha kesi hiyo hadi msajilin wa mahakama atakapoitisha kikao cha kupanga lini kesi hiyo isikilizwe.

SIKILIZA HAPA ILIVYOKUWA................




No comments:

Post a Comment