BAADA
ya Sare ya 0-0 huko Emirates kati ya Arsenal na Manchester United,
Mameneja wa Timu hizo, Arsene Wenger na David Moyes, wamezungumzia Mechi
hiyo.
DAVID MOYES:
-“Ninachoweza kusema ni kuwa tutajaribu
kushinda Gemu yetu ijayo! Kama ipo Klabu ambayo ni wazuri kushinda Gemu
Kipindi cha Pili cha Ligi ni Man United.”
-”Bado Wachezaji wana ari ya ushindi
licha ya kutwaa Mataji mengi. Mmemuona Vidic alivyo mzuri, Rio alikuwa
safi alipoingia. Wote washawahi kuwa Washindi.”
-Akiongelea Robin van Persie kukosa Bao
ambalo lingewapa ushindi: “Lile lingekua Bao safi baada muvu nzuri ya
Rooney lakini Kipa aliokoa!”
ARSENE WENGER:
-“Ilikuwa muhimu tusifungwe! Lakini ilikuwa muhimu tushinde! Nadhani tulikuwa na mchecheto!”
-“Tulitilia mkazo sana Gemu hii pengine
hilo lilituzuia kwenda mbele kushambulia kwa sababu ya zile Goli 5
tulizofungwa Jumamosi!”
+++++++++++++++++++++++
NINI KIJACHO:
Wakati Arsenal wataikaribisha Liverpool
Uwanjani Emirates Jumapili kwenye Mechi ya Raundi ya Tano ya FA CUP, Man
United wao hawana Mechi hadi Februari 22 watakapoenda Ugenini kucheza
na Crystal Palace kwenye Mechi ya Ligi Kuu England, na mwanya huu wa
Siku 10 umewapa nafasi kwenda huko Dubai, Falme za Nchi za Kiarabu,
kupiga Kambi ya Mazoezi ya eneo lenye unafuu kidogo wa hali ya hewa ya
Joto.
MATOKEO:
Jumatano Februari 12
Arsenal 0 Man United 0
Everton v Crystal Palace [IMEAHIRISHWA]
Man City v Sunderland [IMEAHIRISHWA]
Newcastle 0 Tottenham 4
Stoke 1 Swansea 1
Fulham 2 Liverpool 3
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO:
NA | TIMU | P | W | D | L | F | A | GD | PTS |
1 | Chelsea | 26 | 17 | 6 | 3 | 48 | 21 | 27 | 57 |
2 | Arsenal | 26 | 17 | 5 | 4 | 48 | 26 | 22 | 56 |
3 | Man City | 25 | 17 | 3 | 5 | 68 | 27 | 41 | 54 |
4 | Liverpool | 26 | 16 | 5 | 5 | 66 | 32 | 34 | 53 |
5 | Tottenham | 26 | 15 | 5 | 6 | 36 | 32 | 4 | 50 |
6 | Everton | 25 | 12 | 9 | 4 | 37 | 26 | 11 | 45 |
7 | Man United | 26 | 12 | 6 | 8 | 41 | 31 | 10 | 42 |
8 | Southampton | 25 | 10 | 9 | 7 | 37 | 29 | 8 | 39 |
9 | Newcastle | 26 | 11 | 4 | 11 | 32 | 38 | -6 | 37 |
10 | Swansea City | 26 | 7 | 7 | 12 | 33 | 36 | -3 | 28 |
11 | West Ham | 26 | 7 | 7 | 12 | 28 | 33 | -5 | 28 |
12 | Aston Villa | 26 | 7 | 7 | 12 | 27 | 36 | -9 | 28 |
13 | Hull | 26 | 7 | 6 | 13 | 25 | 31 | -6 | 27 |
14 | Stoke | 26 | 6 | 9 | 11 | 27 | 41 | -14 | 27 |
15 | Crystal Palace | 25 | 8 | 2 | 15 | 18 | 34 | -16 | 26 |
16 | Norwich | 26 | 6 | 7 | 13 | 19 | 39 | -20 | 25 |
17 | West Brom | 26 | 4 | 12 | 10 | 30 | 38 | -8 | 24 |
18 | Sunderland | 25 | 6 | 6 | 13 | 25 | 38 | -13 | 24 |
19 | Cardiff | 26 | 5 | 7 | 14 | 19 | 44 | -25 | 22 |
20 | Fulham | 25 | 6 | 2 | 18 | 26 | 58 | -32 | 20 |
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumamosi Februari 22
1545 Chelsea v Everton
1800 Arsenal v Sunderland
1800 Cardiff v Hull
1800 Man City v Stoke
1800 West Brom v Fulham
1800 West Ham v Southampton
2030 Crystal Palace v Man United
Jumapili Februari 23
1630 Liverpool v Swansea
1630 Newcastle v Aston Villa
1900 Norwich v Tottenham
No comments:
Post a Comment