EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Saturday, February 15, 2014

FULHAM YAMCHUKUA FELIX MAGATH, YAMWONDOA RENE MEULENSTEEN!


FELIX_MAGATHRENE MEULENSTEEN, aliekuwa Meneja wa Fulham ambayo iko mkiani kwenye Ligi Kuu England, ameondolewa kwenye wadhifa huo na kupewa aliekuwa Kocha wa zamani wa Bayern Munich Felix Magath.
Katika tamko la Fulham la kutangaza ujio wa Felix Magath, haikusemwa lolote kuhusu hatima ya Meulensteen na inaaminika Mkataba wake unaendelea.
Lakini mwenyewe Meulensteen, ambae aliwahi kuwa Kocha wa Manchester United chini ya Sir Alex Ferguson na ambae alimrithi Martin Jol aliefukuzwa Umeneja Mwezi Desemba na kushinda Mechi 4 tu kati 17 alizosimamia, ameeleza: “Wameweweseka kwa woga…lakini hii ni Soka. Najua Wamiliki wa Klabu walikuwa wakiogopa Timu kushuka Daraja. Tulichojadiliana ni kuendelea kupigana lakini hatua hii ni ya woga. Sijali nini wamesema kwenye tamko lao!”
Katka Taarifa yao iliyotolewa na Mmiliki wa Fulham, Shahid Khan, Raia wa Marekani mwenye Asili ya Pakistan, ilisema: “Zikiwa zimebaki Mechi 12, hakika hatuwezi kukubali kutopokea Matokeo mazuri. Ilibidi hatua ichukuliwe!”

Katika Mechi zao mbili zilizopita za Ligi, Fulham ilifanikiwa kupata Sare ya Bao 2-2 huko Old Trafford walipofanikiwa kusawazisha katika Dakika ya mwisho walipocheza na Manchester United lakini Juzi wakafungwa na Liverpool Bao 3-2 Uwanjani kwao Craven Cottage kwa Bao la Penati ya Dakika ya 90.
Felix Magath, Miaka 60, amesaini Mkataba wa Miezi 18.
Magath ameshatwaa Ubingwa wa Bundesliga mara 3 akiwa kama Meneja na mara ya mwisho ni Mwaka 2009 alipokuwa na Wolfsburg na atakuwa Meneja wa kwanza kutoka Germany kuendesha Klabu ya Ligi Kuu.
+++++++++++++++++++++++++++
Felix Magath
-Alitwaa Bundesliga mara 3 kama Mchezaji akiichezea Hamburg, kati ya Miaka 1978 na 1983, wakicheza pamoja na Nguli wa England, Kevin Keegan
-Mwaka 1983 alitwaa European Cup, akifunga Bao la ushindi dhidi ya Juventus
-Alianza kuwa Meneja Mwaka 1995 akiwa na Hamburg in 1995
-Alitwaa Ubingwa wa Bundesliga akiwa Meneja wa Bayern Munich Mwaka 2005 na 2006
-Alitwaa Ubingwa wa Bundesliga akiwa Meneja wa Wolfsburg Mwaka 2009
+++++++++++++++++++++++++++
Magath amekuwa hana kazi tangu aondoke Wolfsburg Mwaka 2012 na miongoni mwa Kikosi chake cha Timu hiyo kilichotwaa Bundesliga Mwaka 2009 wapo Wachezaji watatu ambao sasa wako Ligi Kuu England ambao ni Edin Dzeko wa Man City na wawili ambao wapo Fulham, Ashkan Dejagah na Sascha Riether.
Magath anatarajiwa kukutana na Wasaidizi wa Meneja wa Fulham, Alan Curbishley na Ray Wilkins, kabla ya kuanza kuitayarisha Fulham ambayo Mechi yao inayofuatia ni Ugenini hapo Jumamosi Februari 22 watakapocheza na West Bromwich Albion ambao wako Nafasi ya 17.

No comments:

Post a Comment