BAO la dakika za lala salama la Mario Balotelli limeipa AC Milan ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Bologna katika mchezo wa Serie A usikuwa jana.
Balotelli alifunga bao lake hilo la 10 msimu huu kwa shuti la umbali wa mita 30 dakika nne kabla ya filimbi ya mwisho na kuipandisha Milan hadi nafasi ya 10 ikifikisha pointi 32 sawa na Lazio iliyo nafasi ya tisa.
Lakini Balotelli alishangilia kigumu bao hilo bila ya kucheka wala kutabasamu, akikikumbatiana tu na wachezaji wenzake.
Balotelli akipongezwa na wenzake baada ya kufunga bao hilo
No comments:
Post a Comment