EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Saturday, February 15, 2014

AZAM FC WATESEKA BARIDI MSUMBIJI


NA MSHAMU NGOJWIKE 
KUFUATIA hali ya hewa ya mvua ya Beira, wachezaji wa Azam Fc wapatiwa vifaa hususani viatu maalum vya kuchezea katika sehemu yenye unyevunyevu.
Azam iko nchini msumbuji leo watashuka dimbani tayari kwa pambanao la marudiano dhidi ya wenyeji Ferroviario da Beira litalokafanyika kwenye uwanja wa wenyeji hao saa 9 alasiri za Msumbiji (saa 10 za Tanzania).
Wawakilishi hao wa Tanzania wanahitaji ushindi au sare kutokana na ushindi wa 1-0 katika mchezo wa kwanza Jumapili iliyopita jijini Dar es Salaam.

 Kikosi cha Azam fc wakiendelea na mazoezi nchini Msumbiji,katika uwanja wa Beira.

Akizungumza na SWACOTZ FORUM kwa mtandoa, Katibu Mkuu wa Azam,  Nassor Idrissa, alisema kuwa hali kama hiyo iliwahi kuwatokea miaka ya nyuma katika maandalizi ya ligi Tanzania bara,wakiwa na uhakika hali hiyo kutoathiri matokeo mabaya ya mechi.
"Tulishakumbana na hali kama hii wakati fulani nchini Uganda wakati tuanajitayarisha na ligi, mazingira yalikuwa magumu sana na tulijikuta tunapigwa na Bunamwaya maboa 4-0, kabla ya mapumziko, kutokana na wachezaji kuteleza ovyo lakini baada ya kubadili viatu tulifanikiwa kurejesha magoli yote na tukapata sare ya 4-4, tokea hapo tumekuwa na tahadhari kubwa ya mambo haya"alisema.

 Mshambuliaji kipre Tche tche kulia akiwa na Keita Raia wa cameroon

Nassor alisema  kulinagana na taarifa zilizokuwa zimepatikana mapema uongozi ulikuwa na dondoo za hali ya hewa ya Beira na hivyo matayarisho muhimu yalifanyika kwa upande wa vifaa hususan uwepo wa viatu maalum vya kuchezea katika sehemu yenye unyevunyevu ili kuhimili utelezi na hatimaye kupata matokeo yanayohitajika.

Katika Mchezo wa Jumapili umepangwa kuchezeshwa na waamuzi kutoka Zambia, Azam  Azam itafaulu kusonga mbele itakabiliana na timu ya Shirika la Umeme la Zambia, Zesco kati ya Machi 1 na 2 jijini Dar es Salaam na kurudiana juma moja baadaye mjini Ndola.


No comments:

Post a Comment