NA MSHAMU NGOJWIKE, DAR
WIMBO mpya unaokwenda
kwa jina la ‘Baby Mbona Umenuna’ wa mwimbaji Mbwana Mohamed maarufu kama Mb
Dogg utakuwa moto wa kuotea mbali, utakapomalizika kurekodiwa katika Studio za
Maccopa.
Mb Dogg ndani ya pozi
Akizungumza na SWACOTZ FORUM, Mkurugenzi wa Kampuni ya Qs Mhonda J Entertainment, Joseph
Mhonda, alisema wimbo huo ambao unaelekea kukamilika utamuweka juu msanii huyo
kutokana na jinsi alivyouandaa
Alisema kwamba Mb Dogg
ni msanii aliyejichimbia kwa muda mrefu akiwa na mahitaji ya kurudi kwenye
nafasi ya juu kama awali, jambo lililomfanya atulie na kufanya kazi ya uhakika.
“Qs inafanya juhudi
kubwa kuleta ile ladha halisi ya msanii huyu aliyetingisha katika anga za
muziki wa Bongo Fleva, enzi hizo akitokea Tip Top ‘Connection’.
Mb Dogg anatokea katika
kampuni hiyo kwa sasa, akiwa sambamba na Nay wa Mitego anayetamba na wimbo wa
Muziki Gani, aliyeimba kwa kushirikiana na Diamond.
No comments:
Post a Comment