ALIYEKUWA kocha Msaidizi wa klabu ya Simba ya Dar es Salaam, Jamhuri Mussa Kihwelo ‘Julio’ ametunukiwa leseni ya daraja B ya ufundishaji kandanda na Shirikisho la Soka Afrika (CAF), baada ya kuhitimu vizuri mafunzo yaliyofanyika mwaka jana visiwani Zanzibar. | ||||||||||||||||||||||||||||||||||
KIHWELU |
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Mwesigwa Selestine leo amemkabidhi Julio leseni yake pamoja na za makocha wote wengine walioshiriki kozi iliyofanyika mjini Zanzibar mwaka jana ambao hawakuwepo.
Makocha wengine waliofuzu kozi hiyo iliyoendeshwa na mkufunzi Bhekisisa Boy Mkhonta kutoka Swaziland ni Abdulghan Msoma, Hafidh Badru, Nasra Juma Mohamed, Gulam Abdallah Rashid, Mohamed Ayoub Suleiman, Shaaban Ramadhan, John Simkoko na Hemed Suleiman Ali. Hivi sasa Tanzania ina makocha 40 wenye leseni B za CAF baada ya wengine 31 kufuzu katika mafunzo yaliyofanyika mapema mwaka juzi jijini Dar es Salaam chini ya mkufunzi Honor Janza kutoka Zambia.
No comments:
Post a Comment