MAREHEMU KISAKA JAMES |
Kisaka amefariki dunia leo asubuhi kwenye hospitali ya Burhan.
James Kisaka alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya macho,kichwa na miguu kwa muda mrefu.
James
Kisaka alizaliwa mwaka 1955 mjini Dar es Salaam na alipata elimu yake
ya Msingi katika shule ya Oysterbay na baadaye sekondari za Mzizima na
Tambaza, Dar es Salaam pia.
Alianza
kupata umaarufu wa soka tangu anasoma na haikushangaza aliposajiliwa na
Sigara akiwa kijana mdogo chini ya umri wa miaka 20.
Baadaye alichezea Nyota Nyekundu, Simba SC, Small Simba ya Zanzibar,
Volcano ya Kenya alipokwenda na Zamoyoni Mogella na LiIa Shomari (pia
marehemu) na Ndovu ya Arusha.
Alikuwemo kwenye kikosi cha Simba kilichokwenda ziara ya mafunzo nchini Brazil mwaka 1981.
Kisaka atakumbukwa kwa upole wake na ufanyaji kazi kwa bidii enzi za uhai wake. Mungu aiweke pema peponi roho ya marehemu. Ami
No comments:
Post a Comment