EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, October 17, 2013

TIMU 56 LIGI DARAJA LA TATU TEMEKE ZATHIBITISHA KUCHUKUA FOMU

NA MSHAMU NGOJWIKE
TIMU 56 za Ligi Daraja la Tatu na Nne za Wilaya ya Temeke Zimethibisha kuchukua fomu huku ikiwa na upungufu wa timu shiriki liogi daraja la tatu.
Ligi  daraja la tatu na nne ngazi ya wilaya ya temeke linarajiwa kuanza novemba 2 amabalo litachezwa kwenye viwanja sita ndani ya wilaya hiyo.
 
Akizungumza na BINGWA Katibu wa Chama cha mpira wilaya ya Temeke(TEFA)Khassim Mustapha Alisema Timu 40 ligi daraja la nne zimechukua fomu hizo, huku timu 16 pekee za ligi daraja la tatu zilizochukua fomu hizo na wakiwa na upungufu wa timu   nne kama kanuni inavyotaka ya kuwa na timu zisizo pungua 18 na zisizo zidi 20.
"hadi sasa na timu za ligi la daraja la nne maana tuna timu 40 na zinatosha kwa ligi yetu, lakini kwa ligi daraja la tatu tuna timu chache hadi  leo timu ambazo zimechukua fomu za ushiriki ni 16 tu" alisema.
Alisema viwanja ambavyo vitatumika kwenye ligi hiyo pamoja na Mzinga jeshini kigamboni,Makangarawe uliopo Yombo,Twalpo Jkt,Mivinjeni wa Shule ya Sekondari Kurasini,Gonga Kongowe na Chamanzi Uliopo Shule ya Msingi Chamanzi.

No comments:

Post a Comment