EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Saturday, July 6, 2013

UNYAMA WAFANYIKA AIRPOT KIBAKA AKAMATWA NA KUPIGWA MPAKA KUUAWA KIKATILI

kassimngumbi.blogspot.com
kibaka aliyekamatwa akiwa na baadhi ya raia wenye hasira wakimtoa bomani kabla ya kifo chake

Kwa mujibu wa maelezo ya mashuhuda (kassian Mpangala) walioko katika eneo la tukio wamesema kuwa mwizi huyo ambaye mpaka saa hizi hajajulikana jina lake alikamatwa majira yasaa kumi na moja alfajiri mitaa ya Jeti kwa Gude Airpot jijini Dar es salaam wakati alipokuwa akijaribu kuiba Redio ndani ya moja ya nyumba ya mkazi wa eneo hilo na muda mfupi baadae wenye nyumba walishtuka hata kabla hajafanikiwa kutimiza tukio lake hilo na walipiga mayowe na kujaza watu nkibao ambao walianza kumshambulia mwizi huyo kwa mawe na magongo ingawa alifanikiwa kuwatoroka na kujificha kwenye boma ambalo linajengwa na baadae wananchi walilizingira boma hilo na kibaka huyo kuzidiwa nguvu,kwa tukio hilo walimtembezea kichapo kilichopelekea kifo chake Askari wa kituo cha polisi cha kati cha Airpot walifika eneo la tukio majira ya saa moja asubuhi na kuukuta mwili wa kibaka huyo ukiwa umetelekezwa mahali hapo huku akiwa `tayari amefariki na hakukuwa na mtu yeyote aliyekutwa eneo la tukio.
AM NOT INVISIBLE - BOLT.
GAZZA AWEKWA LUPANGO KWA ULEVI.
MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa kimataifa wa Uingereza, Paul Gascoigne maarufu kama Gazza amekamatwa baada ya kufanya fujo wakati amelewa katika kituo cha treni. Gazza mwenye umri wa miaka 46 ambaye ametoka kupatiwa matibabu ya kunywa pombe kupindukia nchini Marekani mapema mwaka huu alishikiliwa na polisi baada ya kufanya tukio hilo huko Hertfordshire. Msemaji wa Polisi wa eneo hilo alithibitisha kuwa wamemkamata nyota huyo wa zamani baada ya kupigiwa simu na mlinzi wa eneo la kituo cha treni kwamba anafanya fujo kutokana na kulewa pombe kupitiliza. Msemaji huyo aliendelea kudai kuwa walimshikilia Gazza kwa saa 12 na baadae kuwekewa dhamana na uchunguzi wa polisi unaendelea kuhusiana na tukio hilo kabla ya kupelekwa mahakamani. Mapema mwaka huu baadjhi ya wachezaji walijichangisha na kupata fedha ambazo zilimsadia Gazza kumpeleka Marekani kwa ajili ya matibabu ya kuzuia ulevi uliopindukia baada ya hali yake kuwa mbaya.
WACHEZAJI WAWILI WA SERIE A WAFUNGIWA NA FIFA KWA KUPANGA MATOKEO.
WACHEZAJI wawili wa vilabu vya Ligi Kuu nchini Italia marufu kama Serie A wamefungiwa miezi mitatu na siku 10 na kutozwa faini ya euro 10,000 kila mmoja baada ya kukutwa na hatia ya kutengeneza mikakati ya kupanga matokeo ya mechi zao. Wachezaji ambao ni mshambuliaji wa klabu ya Torino, Paulo Vitor de Souza Barreto na beki wa klabu ya Genoa Giovanni Marchese walitandikwa adhabu hiyo na Shirikisho la Soka nchini Italia baada ya kushindwa kujitetea kutokana na tuhuma hizo. Mbali na hao IFF pia ilimfungia Davide Lanzafame ambaye anacheza kwa mkopo katika ya Honved ya Hungary akitokea klabu ya Catania, miezi 16 na faini ya euro 40,000 baada ya yeye pia kukutwa na hatia katika makosa ya kupanga matokeo wakati akiwa Italia. Hukumu hiyo imetolewa bada ya kufanyika uchunguzi katika mechi zilizohusisha timu ya Bari katika msimu wa 2008-2009 wakati ikiwa daraja la pili na msimu wa 2010-2011 wakati ikiwa ligi kuu.

No comments:

Post a Comment