EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Saturday, July 6, 2013

MSANII DIAMOND ASABABISHA KIFO MWANANYAMARA



Vilio  na  simanzi  vilitanda Jumatano iliyopita Mwananyamala Kisiwani, jijini Dar kufuatia mtoto wa mwaka mmoja, Rahim Rajab kufariki dunia kwa kuangukiwa na watu watatu, akiwemo baba yake mzazi, Rajab Said.. Tukio la watu hao kumwangukia mtoto huyo lilitokea Jumatatu iliyopita na lilisababishwa na ugomvi mkubwa wa CD yenye nyimbo za mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ulioibuka ndani ya chumba cha kulala kati ya mama wa marehemu na mpangaji mwenzake aitwaye Aisha. Akizungumza kwa machungu kuelezea tukio hilo, mama mzazi wa marehemu Rahim, Habiba Ally alikiri kuwa kisa cha kifo cha mwanaye ni...

NELSON MANDELA YUKO KATIKA HALI YA "USINGIZI WA KUDUMU"....NYARAKA ZAFICHUKA


Nelson Mandela ameendelea kuwekwa hai kwa msaada wa mashine za kumsaidia kupumua na  'anakaribia kifo,' nyaraka za mahakama zimefichua. Afya ya rais huyo wa zamani ni 'yenye hatari kubwa,' kwa mujibu wa nyaraka zilizowasilishwa mahakamani kwenye kesi ambayo imepelekea mabaki ya miili ya watoto wake watatu kuzikwa upya Alhamisi kwenye makaburi yao ya awali.   Nyaraka za mahakama za Juni 26 zilisema: "Matarajio hayo ya kukaribia kifo chake yanaegemea katika uhalisia na uthabiti,' zilisema nyaraka hizo za mahakama.  Mandela, ambaye alilazwa hospitali Juni 8, ameendelea kuwa mahututi lakini hali inayoimarika, kwa mujibu...

LOWASSA AVIONYA VYOMBO VYA DOLA...!



WAZIRI Mkuu mstaafu, Edward Lowassa amevitaka vyombo vya dola na wafanyabiashara wakubwa nchini, kujenga mahusiano bora kati yao na wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga) ili kuondoa tabaka la matajiri na masikini linaloweza kuathiri uchumi wa taifa. Lowassa aliyasema hayo jana wakati akizungumza na machinga wa eneo la Makoroboi jijini Mwanza, ambao pamoja na mambo mengine aliwachangia sh milioni 20 kwa ajili ya kutunisha mfuko wao. Mwanasiasa huyo ambaye pia ni mbunge wa Monduli, aliinyoshea kidole Serikali ya chama chake cha Mapinduzi (CCM) na kuitaka ihakikishe inatekeleza kwa vitendo ilani yake inayosisitiza wananchi kuwezeshwa...

PICHA ZA LAANA ZA KUNDI LA BAIKOKO - TANGA


Hizi  ni  baadhi  ya  picha  za  kundi  la  wacheza  uchi / nusu  uchi  maarufu  kwa  jina  la  Baikoko  lenye  maskani  yake Tanga....        ...

PICHA CHAFU ZA MISS UNIZIK ZASAMBAA MITANDAONI....


Vituko  vya  mapenzi  ya  Tz kumbe  hata  nchi  za  nje  vipo..!! Huyu  ni  denti  wa  chuo  kikuu  cha  UNIZIK  kilichoko Nigeria  ambaye  pia  ni miss  UNIZIK 2013/2014.... Mrembo  huyu  amekutana  na  balaa  hili  baada  ya  mpenzi  wake  kuzisambaza  picha  zake  za  utupu.... Taarifa  toka  chuoni  hapo  zinadai  kuwa,  wapenzi  hao  walizunguana  siku  kadhaa   baada  ya  mrembo  huyo ...

"MWANAUME ASIYE NA PESA HAPASWI KUWA NA WIVU KWA MPENZI WAKE"....JINI KABULA


 MSANII wa filamu za Bongo, Miriam Jolwa ‘Kabula’ ameonesha kukerwa na wanaume ambao hawana hela   lakini wamekuwa wakijifanya wanajua kupenda sana huku wakiwa na wivu kupitiliza. Akiongea na  mwandishi wetu , Kabula alisema anajua kupenda ni suala la msingi lakini anawashangaa wale wanaokuwa na wivu wa kupindukia na wakati mwingine kutoa vipigo kwa wapenzi wao wakati wao ni wanaume  wasio na kitu. “Unajua nawashangaa sana wanaume wa aina hiyo, wanakuwa na wivu kupitiliza lakini hawawasaidii chochote wapenzi wao kifedha  zaidi ya kuonesha wana wivu  na wakipishana kidogo tu kipigo kinatembea, mimi...

WAZIRI MAGUFULI ATAMANI KUWA RAIS WA TANZANIA......ANADAI KWAMBA YUPO TAYARI KUGOMBEA MWAKA 2015 ENDAPO ATAKIDHI MASHARTI


 Katika hali inayoonyesha kuwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, anautamani urais, amesema anaweza kutangaza nia hiyo kama atakidhi masharti yatakayowekwa kwenye Katiba mpya. Alisema iwapo Katiba ijayo itakuja na sifa ambazo atakidhi vigezo kuna uwezekano mkubwa wa kuwania nafasi hiyo na kwamba iwapo atapungukiwa sifa zinazohitajika kwa mujibu wa Katiba hataingia kwenye kinyang’anyiro hicho. Dk. Magufuli ambaye pia ni Mbunge wa Chato alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wazee wa wilaya hiyo kwenye ukumbi wa ‘Mshikamano Saccos’, muda mfupi baada ya mzee Paschal Nyambibo (87) kumsihi agombee nafasi hiyo mwaka 2015 kutokana...

SH. 500/- SASA ITAKUWA SARAFU BADALA YA NOTI ILI KUIFANYA ISICHAKAE HARAKA


KUTOKANA na kuchakaa haraka kwa noti ya shilingi 500 na kiwango chake kudumu kwenye mzunguko kwa miezi sita tu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imesema inatarajia kubadili noti hiyo na kuwa ya sarafu.Akizungumza na gazeti la Tanzania Daima juzi  kwenye viwanja vya maonesho ya kimataifa ya biashara, jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Fedha, Abdul Dollah, alisema mabadiliko hayo yatafanyika hivi karibuni na sarafu hiyo itadumu kwenye mzunguuko kwa zaidi ya miaka 20 huku ikiwa na ubora wake.Dollah alitaja sababu nyingine ya uchakavu huo ni kutokana na noti hiyo kushikwa na watu wengi kwenye mzunguko huku baadhi yao wakishindwa...

"WIMBO WA MAJANGA UMENIPA DILI LA KUREKODI MOVIE AFRIKA KUSINI "– SNURA.


 MWIGIZAJI wa kike na mwimbaji wa muziki wa kizazi kipya Snura Mushi amedai kuwa muziki ulimpa dili ya kwenda kurekodi filamu Afrika ya Kusini... Anasema kuwa dili hilo  amelipata kutokana na  kufanya vizuri katika muziki hasa nyimbo yake ya Majanga. “Filamu kwa sasa inachangamoto sana .Hilo lilinifanya nirudi katika muziki huku nikichagua filamu za kuigiza na kujikita katika muziki zaidi ambao unanifanya niwe bussy sana.. " Lakini ninachofurahia kupitia nyimbo yangu ya majanga nilipoenda kuirekodia Afrika kusini Nnilipewa uhusika mkuu kuigiza filamu ya Tandeka,”anasema Snura. Snura anadai kuwa watayarishaji walimuona...

FBI WAINGIA ARUSHA KUCHUNGUZA BOMU LA SOWETO


  Askari wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI), tayari wapo Arusha kushirikiana na polisi ili kuchunguza tukio la mlipuko wa bomu la kutupa kwa mkono kwenye mkutano wa kampeni za Chadema. Katika tukio hilo lililotokea Juni 15, mwaka huu Viwanja vya Soweto, eneo la Kaloleni, Arusha, watu wanne walipoteza maisha huku zaidi ya 60 wakijeruhiwa. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Lebaratus Sabas, alithibitisha ushiriki wa FBI katika upelelezi huo. Licha ya FBI, polisi wanashirikiana na wenzao kutoka nchi jirani ya Kenya, ambao wana uzoefu na matukio ya milipuko ya mabomu yanayotokea nchini mwao mara kwa mara, hasa baada ya nchi...

BOMOA BOMOA YA POMBE MAGUFULI YAANZA.....JENGO LA BUSINESS PARK ( GREEN ACRES ) LABOMOLEWA


 Baada Waziri wa Ujenzi, Pombe Magufuli kutoa maagizo kwa wenye majengo yaliyo pembezoni mwa barabara ya Ali Hassan Mwinyi, kubomoa wenyewe majengo yao ili kupisha upanuzi wa barabara hiyo, kuonekana yakisua sua, hatimaye leo ameanza rasmi kazi ya kubomoa kwa Greda katika majengo ya wale walioonekana kukaidi agizo hilo.  Katika kutekeleza agizo hilo zoezi hilo limeanzia kwenye Jengo la Business Park (Green Acres) lililopo eneo la Victoria ambapo hadi hivi sasa zoezi hilo bado linaendelea pande hizo chini ya usimamizi ya Askari  Msongamano pande hizo.....  Tayari ukuta ukiwa umeshashushwa...

No comments:

Post a Comment