Thomasi Ulimwengu |
Akizungumza Kutoka nchini kenya , Ulimwengu aliye kwenye kikosi cha Bara, Kilimanjaro Stars kinachoshirki Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge amesema kwamba ana matumaini makubwa ya kuhamia Ulaya.
“Nina ofa nyingi na zinafanyiwa kazi kwa sasa, nadhani muda si mrefu nitaondoka Afrika, tuombe Mungu,”alisema mshambuliaji huyo wa Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Ulimwengu anacheza klabu moja na Mtanzania, mwenzake Mbwana Ally Samatta, TP Mazembe na wote kwa sasa ndiyo wachezaji wakubwa zaidi na tegemeo wa Tanzania.
No comments:
Post a Comment