Pumzika kwa amani baba wa Taifa |
"Taifa letu limepoteza mtoto wake mkubwa. Watu wetu wamepoteza baba",".
Pumzika kwa amani shujaa; Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amethibitisha Nelson Mandela amefariki akiwa na umri wa miaka 95Nelson Rolihlahla Mandela alizaliwa Julai 18, mwaka 1918 na ndiye rais wa kwanza aliyechaguliwa kidemokrasia nchini Afrika Kusini.
Alikuwa mwanasheria na mwanachama wa ANC aliyepinga siasa ya ubaguzi wa rangi Apartheid katika Afrika Kusini.
Mandela alitumikia kifungo cha maisha kwa miaka 27 kutokana na harakati zake za kuupinga ubaguzi wa rangi.
Alifungwa katika kisiwa cha Robben. Baada ya kuachiwa huru mwaka 1990 alianzisha sera ya maridhiano. Mwaka wa 1993, pamoja na Frederik Willem de Klerk alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Amani.
No comments:
Post a Comment