INGAWA Meneja wa Manchester United David
Moyes amedai maumivu ya Robin van Persie si kitu cha kutisha na kikubwa
lakini ameshindwa kutaja ni lini Staa huyo atarudi dimbani kuiokoa Man
United ambayo Jumamosi itacheza bila ya nguzo yao muhimu Wayne Rooney.
Van Persie ameshazikosa Mechi 4 za Man
United akijiuguza maumivu ya Nyonga na mara ya mwisho kucheza ni pale
alipoitungua Klabu yake ya zamani Arsenal ambayo ilifungwa Bao 1-0 kwa
Bao lake.
Tangu Van Persie akose Mechi hizo 4, Man
United imeambua Pointi 2 tu katika Mechi 3 za Ligi ingawa waliichabanga
Bayer Leverkusen Bao 5-0 kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI huko Ujerumani.
No comments:
Post a Comment