GWIJI wa soka duniani,
Pele hatashiriki droo ya upangaji ratiba ya Kombe la Dunia
itakayofanyika Leo, baada ya kukataa fursa hiyo akihofia kuiweka
Brazil katika kundi gumu. Pele amesema atakuwepo kushuhudia zoezi hilo
lakini amethibitisha hatashiriki. Nguli aliendelea kudai kuwa rais wa
Brazil Dilma Rousseff alimpendekeza aiwakilishe nchi hiyo litakapokuja
zoezi la kuchagua timu na kuweka katika makundi kazi ambayo ameifanya
mara kadhaa. Pele amesema ameamua kukataa kwasababu asingejisikia vyema
kuchagua timu ambazo zitaiweka Brazil mahali pagumu. Droo ya kupanga
ratiba ya michuano hiyo itakayoanza kutimua vumbi Juni 12 mwakani
itashirikisha nchi 32 kutoka sehemu mbalimbali duniani.
No comments:
Post a Comment