EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Monday, October 28, 2013

WACHEZAJI WA NGUMI NCHINI WAONDOKA LEO KUELEKEA IRAN KATIKA MICHUANO YA DUNIA

Kaimu Katibu wa Zurkhaneh  Tanzania Abdallah Nyoni
NA MSHAMU NGOJWIKE
 
WACHEZAJI wa mchezo wa ngumi unaofahamika kama Zurkhaneh wameondoka hii leo kwenda nchini Iran kwenye mashindano ya Dunia ambayo yataanza kuchezwa Oktoba 30 hadi Novemba 3.
Mashindano hayo  yatashirikisha nchi 25 wanachama wa mchezo huo,huku Afrika zikiwakirishwa za Tanzania,Kenya,Uganda,Msumbiji,Benin,Zambia na Zimbabwe.
Akizungumza na waandishi wa habari  Kaimu Katibu wa Zurkhaneh  Tanzania Abdallah Nyoni amesema vijana hao wametoka asubuhi ya leo kuelekea nchini Iran ambako kutafanyika Mashindano hayo kwenye Mji wa Lorestan huku wakiwa na murali ya kurudi na ushindi kutegemeana na mazoezi waliyofanya.
Alisema mwaka huu kwenye fainali hizo zitawakilishwa na Mwarabu Mirundi pamoja na Patrick Ntakisigaye kutoka kwenye klabu ya Mianzini zurkhaneh iliyopo Mbagala Dar es Salaam.
Mashindano hayo ya Zurkhaneh  kwa upande wa Koshti Pahlavani yameandaliwa na nchi ya Iran ambayo yamedhaminiwa na International Zurkhaneh sports Federation(IZSF).

No comments:

Post a Comment