EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Tuesday, October 22, 2013

MTWARA WAHIMIZWA KUSHIRIKI KILIMO



Imeelezwa kuwa ni vizuri wananchi wa manispaa ya mtwara mikindani wakajitoa zaidi kwenye kilimo, ili kuondoa tatizo la baa la njaa, ambalo limeanza kujitokeza kwa majirani zetu wa mkoa wa lindi.


Hayo yamesemwa na wananchi tofauti tofauti wakati wakizungumza na mwandishi wa habari wa pride fm radio mapema hii leo asubuhi, ambao wamesema kuwa tatizo ambalo linaanza kuonekana mkoa wa lindi linaweza kufika mkoani mtwara hivyo ni vizuri kujipanga mapema kwa ajili ya kukabiliana na tatizo hilo.
Baadhi ya wananchi waliozungumza na pride fm radio akiwemo godfrey namohochi wa manispaa ya mtwara mikindani amesema kuwa kila mwaka nchi huwa inaingia kwenye janga la njaa, tatizo ambalo husababishwa na wananchi kutojikita katika kilimo.



Mkazi mwingine mkata juma amesema kuwa kutokana na kutozalisha tunaendelea kuilaumu serikali kuwa haitoi misaada hivyo akawaomba wananchi kujikita katika kuzalisha mazo kutokana na msimu wa mvua kuanza hali ambayo itatutoa kwenye majanga ya kutokuwa na chakula cha kutosha.
Naye juma hamisi amewataka wananchi wenzake kuwa waelewa na kufuata ushauri na elimu inayotolewa na wataalamu wa kilimo ili kujikwamua kiuchumi na hata kuondoa janga la njaa ambalo huwa linajitokeza mara kwa mara na kupunguza mzigo kwa serikali.

No comments:

Post a Comment