EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Monday, October 28, 2013

JAMALI MALINZI AANZA UONGOZI KWA KUFULU KWA WAJUMBE WAKE WAPYA

 
Jamali malinzi -Raisi mpya TFF
NA MSHAM NGOJWIKE
RAIS Mpya wa Shirikisho la Soka Nchini  (TFF), Jamal Malinzi amewazawadia wajumbe wa mkutano mkuu ofa ya kuendelea kubaki jijini Dar es Salaam kwa siku moja zaidi ikiwa ni pamoja na kuwalipa posho.
Awali wagombea hao walitakiwa kuondoka jijini jana na kurejea makwao kufuatia kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo uliofanyika juzi na kumalizika usiku wa manane katika ukumbi wa Waterfront jijini Dar es Salaam.
 Akizungumza mara baada ya kuachiwa kiti hicho cha urais kutoka kwa Leodegar Tenga aliyekaa madarakani toka 2005 – 2013, Malinzi alimwaga cheche pale alipotamka kutoa ofa ya wajumbe kuendelea kubaki jijini kwa siku moja huku akiahidi kulipa gharama za hoteli waliyofikia ya Landmark pamoja na posho zao.
 
“Mbali na kukaa katika hotel hiyo kwa siku moja zaidi nawapa ofa pia ya kuwapa posho yao ya mda huo mpaka watakapoondoka siku inayofuata kwani watakuwa wamechoka kutokana na uchaguzi kumalizika usiku wa manane, ”alisema.
 
Alisema pia anamshukuru mpinzani wake Athuman Nyamlani kwa kufanya kampeni za amani bila ya kuchafuana hivyo kuwa tayari kushirikiana naye pamoja na wengine wote katika kuendeleza soka la Tanzania.
 
 
“Natoa pia shukrani kwa wajumbe wote wa  mkutano mkuu wa uchaguzi 2013 kwa kunikubali na hata wale walionipinga kwani ndiyo demokrasia, kwa ujumla nawashukuru kwa kunipa dhamana ya kuwa Rais wa TFF,”alisema
 
Aliongeza: “Kweli dunia imekuwa kijiji, kwani kipindi cha masaa 72 baada ya kuzindua ilani yangu ya uchaguzi, nimepokea salamu, maoni na mapendekezo toka ndani na nje ya Tanzania ikiwa ni pamoja na Burundi, Ivory Coast, Denmark na NewZealand, nitatumia vizuri mawazo hayo kujenga soka letu”alisema.

No comments:

Post a Comment