NA MSHAMU NGOJWIKE
TIMU ya Ndanda , jana imekabidhiwa msaada wa vifaa vya michezo kutoka kwa Kampuni ya Gesi
ya BG Tanzania ya Mtwara .
Vifaa hivyo vimekabidhiwa kwa ajili ya kutumiwa katika
maandalizi ya Ligi Kuu soka Tanzania bara inayotarajia kuanza Septemba 20.
Vifaa vilivyokabidhiwa
na Meneja Kampuni hiyo Adam
Prince ni Viatu, Mipira 20 aina ya Brazuka, Jezi pea 30, jaketi 30,traki suti za mazoezi pea 30.
Pia, alisema watakabidhi basi jipya aina ya Toyota lenye uwezo
wa kubeba wachezaji 30 ifikapo Novemba mwaka huu, mara baada ya kufika nchini.
Akizungumza katika Hafla ya kukabidhi vifaa hivyo, Meneja huyo
alisema wanajisikia faraja kupokelewa vizuri
Mtwara, wanataka kuifanya Ndanda
kuwa timu tishio kwenye msimu wa ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
“Tumefanya hivi kujiweka karibu na jamii, nakuifanya Klabu ya
Ndanda kuwa miongoni mwa timu tishio kwenye msimu mwa huu wa Ligi Kuu Tanzania
Bara,”alisema.
Mkuu wa Mkoa wa
Mtwara,Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia amewataka wachezaji pamoja na wadau
wengine kujitokeza kuisaidia timu hiyo ili ifanye vizuri kwenye msimu wa Ligi
Kuu mwaka huu.
“Ninawashukuru BG Tanzania kwa Msaada wao huu,hii ni kuonyesha
jinsi gani wanavyothamini watu wao wa Mtwara,ninawataka na wadau wengine
kuisaidia timu yetu,”alisema.
Ndanda FC ipo jijini hapa, imeweka kambi ya siku
40,kwenye Chuo Cha Kikuu Cha Ardhi
ikijiandaa na Ligi kuu Msimu ujao.
Wanariadha
wa Tz kurekebisha rekodi michuano ya Kitaifa
i
No comments:
Post a Comment