WANARIADHA
wa Tanzania wamepanga kuyatumia mashindano ya majeshi ya Afrika Mashariki
yanayotarajia kuanza keshokutwa Zanzibar
kurekebisha rekodi za muda wao kitaifa.
Akizungumza
na SWACOTZ FORUM jana Katibu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Suleiman Nyambui
alisema mashindano hayo hayatambuliwi na Shirikisho la Riadha la Kimataifa
(IAAF) lakini ni fursa nyingine kwa wanariadha wa Tanzania walioajiliwa na
Taasisi za vyombo vya Ulinzi na Usalama kujipima nguvu kwa Wakenya na Waganda.
Nyambui
alisema RT sio msemaji wa mashindano hayo lakini inachokijua ni kwamba ni
mashindano muhimu kwa taasisi za jeshi
hivyo lazima yatawashirikisha wanariadha wa wenye uwezo mkubwa ili kuhakikisha
kila chombo cha ulinzi na usalama kinapata ushindi.
“Japokuwa
mashindano hayo hayaingiliani kabisa na RT lakini ni muhimu kwetu maana tuna
uhakika kila jeshi limewaandaa vizuri wanariadha wake ili kuhakikisha wanafanya
vizuri jambo ambalo litawasaidia kurekebisha muda wao wa ndani,” alisema.
Alisema
hakuna wanariadha anayetaka kufungwa ila cha msingi wanatakiwa kurekebisha muda
wao kwa kujipima nguvu na wakimbiaji mashuhuri kutoka Kenya na Uganda ambao
wamekuwa wakifanya vizuri katika michuano ya kimataifa.
No comments:
Post a Comment