|
MZE MASOUD AHMAD..BABA MZAZI WA MCHEZAJI ABDALLAH MASOUD WA AZAM NA TIM YA TAIFA |
NA:KASSIM NGUMBI...........Mtwara
Mzee
Masoud Ahmad Athumani Baba Mzazi Wa Mhezaji
Nyota Chipukizi Anayechezea Klabu Ya Azam Fc Kwa Sasa Abdallah Masoud (DULLA)
Ametoa Shukrani Zake Za Dhati Kwa Uongozi Wa Wilaya Ya Mtwara Vijijini Upande
Wa Michezo Kwa Kumtoa Kijana Wake Na Hatimaye Hivi Sasa Amefikia Kiwango Cha
Kuchezea Timu Ya Taifa Mze Masoud Aliiambiaswacotz FORUM Ilipomtembelea
Kijijini Kwake Msimbati Mtwara Vijijini Kuwa Dulla Alizaliwa Katika Kijiji Cha
Msimbati Na Alilelewa Hapo Harakati Za Soka Alizianza Toka Akiwa Mdogo Ambapo
Alikua Akichezea Timu Za Shule Toka Shule Ya Msingi Mpaka Amefikia Sekondari
Ambapo Sasa Ana Umri Wa Miaka 17 Baada Ya Juhudi Zake Za Soka Kuonekana Katika
Ushiriki Wa Michuano Ya Umiseta Baadaye Uongozi Wa Wilaya Ulimhamisha Na
Kumpeleka Mtwara Mjini Ambako
|
MZE MASOUD |
Alianza Kuchezea Timu Ya Vijana Iitwayo COAST Na
Baada Ya Hapo Mwaka Jana Aliondoka Na Kuelekea Azam Fc Ambako Alipokelewa Na
Mpaka Sasa Yupo Huko,Pia Amesema Kuwa Mpaka Sasa Yeye Na Kijiji Kizima Kwa
Ujumla Wamekuwa Wakijisikia Faraja Sana Kuona Kwamba Wana Uwakilishi Kubwa
Katika Klabu Kubwa Pamoja Na Timu Ya Taifa Na Pia Wanaamini Kuwa Kijana Wao
Ataendelea Kufanya Vizuri Katika Tathnia Ya Soka Hapa Nchini Na Nje Ya Nchi
Kwani Bado Wanamuombea Mungu Aweze Fanya Vizuri Zaidi Ya Hapo Alipo Sasa.
No comments:
Post a Comment