KATIKA hali
inayoonesha Umakini wa Chama cha Chadema kusimamia maamuzi yake ya
kuachana na ajenda za Wasaliti ili kisitoke kwenye hoja muhimu, sasa
kimejikita kwenye mikakati mizito ya 2014, ambapo jana wanachama 35 wa
Chama Tawala (CCM) wamejiunga na CHADEMA.
Wanachama
hao wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ni wale wa Kijiji cha Kisala wilayani
Mvomero, ambao katika Kijiji chao Ng’ombe zaidi ya 15 walikatwa miguu ya
mbele na ya nyuma na kuwa Vibutu kutokana na vurugu za wakulima na
wafugaji.
Wakizungumza
katika mkutano huo, Mgombea Udiwani wa Kata ya Sungaji 2010, Jairos
Msigwa, aliwataka wananchi waachane na Propaganda za CCM na kujiunga na
CHADEMA akidai kwamba,
“Wakati CCM
kimeacha kushughulikia Sera Mbovu ya Wakulima na Wafugaji na badala yake
kueneza Usaliti ndani ya Chadema, chadema kimejikita kutatua kero zenu
na maazimio ya ajenda sita za chama, ikiwa ni pamoja na bei ya Umeme
iliyoanza kuwaumiza na Katiba”.alisema Msigwa.
Diwani wa
Viti Maalum (Chadema), Juliana Petro, aliwataka akina mama kuondokana na
woga wa kudai haki zao, alikumbusha kuna ujanja ujanja wa viongozi
kuhusu kero ya Daraja la Kisala akidai hakuna fedha iliyotengwa na hadi
leo wanateseka licha kuambiwa kila siku.
Aidha Diwani
wa Kata ya Mtibwa, Luka Mwakambaya, aliwashauri wananchi, kwenye
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mwaka huu (2014), waondokane na Viongozi
wababishaji wasiokuwa na dhamira kuwasaidia, na badala wawachague
viongozi makini wa chama chake, ambao watalinda haki zao.
SOURCE:CHADEMA BLOG
No comments:
Post a Comment