GOLIKIPA nyota wa klabu
ya Bayern Munich, Manuel Neuer amesema amefurahishwa kuwa golikipa pekee
kuchaguliwa kugombea tuzo ya mchezaji bora wa dunia maarufu kama Ballon
d’Or mwaka huu. Neuer
ni mmoja kati ya wachezaji sita wa Bayern walioingia katika orodha hiyo
ya wachezaji 23 baada ya timu hiyo kufanikiwa kushinda mataji matatu
mfululizo katika msimu wa 2012-2013. Akihojiwa
Neuer amesema ni heshima kubwa kwake kuwa golikipa pekee aliyepata
nafasi hiyo na wote wanategemea kwamba mchezaji mojawapo katika Bayern
ndiye atakayeibuka kidedea katika tuzo hizo. Bayern
ambayo msimu uliopita ilikuwa ikinolewa na Heynckes, imeendelea kuwa
katika kiwango cha juu chini ya kocha mpya Pep Guardiola toka kuanza kwa
msimu mpya na Neuer ameeleza kufurahishwa na jinsi wanavyocheza hivi
sasa.
No comments:
Post a Comment