ZIKIWA
zimebaki Mechi 3 ili hatua ya Makundi imalizike, Cristiano Ronaldo
anahitaji Bao moja tu ili afikie Rekodi inayoshikiliwa kwa pamoja na
Ruud van Nistelrooy, Filippo Inzaghi na Hernán Crespo ya kufunga Mabao mengi kwenye Hatua za Makundi za UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Msimu huu, Ronaldo ameshapiga mabao 7 akiwa na Real Madrid ambao wamefunga Bao 12 katika Mechi 3.
Ruud van Nistelrooy, Filippo Inzaghi na Hernán Crespo, walifunga mabao yao 8 Hatua za Makundi Msimu wa 2004/05 kwa Van Nistelrooy, 2002/03 kwa Crespo na Inzaghi.
- BAADHI YA NYOTA AMBAO WALIKARIBIA REKODI HIYO KWENYE HATUA ZA MAKUNDI:
2013/14: Ronaldo (7), Ibrahimovic (6) –
2012/13: Burak and Ronaldo (6)
2011/12: Gomez and Messi (6)
2010/11: Eto'o (7)
2009/10: Ronaldo (6)
2008/09: Benzema, Gerrard, Klose, Messi (5)
2007/08: Ibrahimovic, Ronaldo (5)
2006/07: Drogba, Kaká, Morientes (5)
No comments:
Post a Comment