Sep 24, 2013
*AMKUMBATIA RAIS KIKWETE NA KUMWITA 'KAKA NA RAFIKI WA KWELI'
MAREKANI
Rais wa Marekani Mheshimiwa Barack Obama ametoa pongezi na sifa kwa Tanzania kwa kuwa miongoni mwa nchi chache duniani ambazo zimetia saini mkataba wa Ushirikiano wa Serikali Zinazoendeshwa kwa Uwazi ambao unalenga kujenga na kuendeleza nafasi ya taasisi zisizokuwa za Kiserikali katika utawala bora, uwazi na uwajibikaji katika uendeshaji wa Serikali.
Rais Obama ametoa pongezi hizo kwa Tanzania leo, Jumatatu, Septemba 23, 2013, wakati akizungumza katika mkutano maalum aliouandaa mwenyewe Rais Obama kuzungumzia nafasi za Serikali katika kuunga mkono na kuendeleza asasi na taasisi zisizokuwa za Kiserikali na kuzishirikisha zaidi katika kuboresha shughuli za utawala bora uliofanyika kwenye Hoteli ya Hilton, mjini New York, Marekani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alikuwa miongoni mwa viongozi wachache duniani walioalikwa kushiriki mkutano huo maalum ambao pia ulishirikisha wawakilishi wa asasi zisizokuwa za Kiserikali 300.
Baadhi ya nchi nyingine za Afrika zilizoalikwa na kushiriki katika mkutano huo ni pamoja na Liberia, Ghana, Benin, Libya, Tunisia, Senegal, Afrika Kusini na Botswana.
Shabaha kuu ya mkutano huo wa saa moja ilikuwa ni kutafuta namna ya kuongeza kiwango cha kuungwa mkono kwa taasisi na asasi hizo na jinsi gani ya kuzilinda ili kuziwezesha kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Aidha, mkutano huo ulilenga kuzitaka Serikali ambazo zinaweka vikwazo kwenye utendaji wa asasi hizo kuondoa vikwazo hivyo haraka ambavyo vinahujumu utendaji kazi na mchango wa asasi hizo katika uendeshaji wa utawala bora.
Katika hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo, Rais Obama amezisifia nchi kama Tanzania ambazo zimetia saini makubaliano ya Ushirikiano wa Serikali Wazi ambayo yanalenga kupandisha nafasi ya asasi zisizokuwa za Kiserikali katika Utawala Bora,Uwazi na Uwajibikaji katika Serikali.
Amesema kuwa binafsi alikuwa ameamua kukutana na viongozi wa asasi zisizokuwa za kimataifa wakati wa ziara yake ya karibu katika Afrika ambako miongoni mwa nchi nyingine alitembelea Tanzania.
Rais Obama alifurahi sana kukutana na Rais Kikwete. Rais Obama alimkumbatia Rais Kikwete akimwelezea kama “kaka wa karibu na rafiki mzuri” kauli na kitendo ambacho kiliwashangaza mamia ya watu waliokuwa kwenye ukumbi.
Maktaba: Rais Obama na Rais Jakaya Kikwete |
Rais wa Marekani Mheshimiwa Barack Obama ametoa pongezi na sifa kwa Tanzania kwa kuwa miongoni mwa nchi chache duniani ambazo zimetia saini mkataba wa Ushirikiano wa Serikali Zinazoendeshwa kwa Uwazi ambao unalenga kujenga na kuendeleza nafasi ya taasisi zisizokuwa za Kiserikali katika utawala bora, uwazi na uwajibikaji katika uendeshaji wa Serikali.
Rais Obama ametoa pongezi hizo kwa Tanzania leo, Jumatatu, Septemba 23, 2013, wakati akizungumza katika mkutano maalum aliouandaa mwenyewe Rais Obama kuzungumzia nafasi za Serikali katika kuunga mkono na kuendeleza asasi na taasisi zisizokuwa za Kiserikali na kuzishirikisha zaidi katika kuboresha shughuli za utawala bora uliofanyika kwenye Hoteli ya Hilton, mjini New York, Marekani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alikuwa miongoni mwa viongozi wachache duniani walioalikwa kushiriki mkutano huo maalum ambao pia ulishirikisha wawakilishi wa asasi zisizokuwa za Kiserikali 300.
Baadhi ya nchi nyingine za Afrika zilizoalikwa na kushiriki katika mkutano huo ni pamoja na Liberia, Ghana, Benin, Libya, Tunisia, Senegal, Afrika Kusini na Botswana.
Shabaha kuu ya mkutano huo wa saa moja ilikuwa ni kutafuta namna ya kuongeza kiwango cha kuungwa mkono kwa taasisi na asasi hizo na jinsi gani ya kuzilinda ili kuziwezesha kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Aidha, mkutano huo ulilenga kuzitaka Serikali ambazo zinaweka vikwazo kwenye utendaji wa asasi hizo kuondoa vikwazo hivyo haraka ambavyo vinahujumu utendaji kazi na mchango wa asasi hizo katika uendeshaji wa utawala bora.
Katika hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo, Rais Obama amezisifia nchi kama Tanzania ambazo zimetia saini makubaliano ya Ushirikiano wa Serikali Wazi ambayo yanalenga kupandisha nafasi ya asasi zisizokuwa za Kiserikali katika Utawala Bora,Uwazi na Uwajibikaji katika Serikali.
Amesema kuwa binafsi alikuwa ameamua kukutana na viongozi wa asasi zisizokuwa za kimataifa wakati wa ziara yake ya karibu katika Afrika ambako miongoni mwa nchi nyingine alitembelea Tanzania.
Rais Obama alifurahi sana kukutana na Rais Kikwete. Rais Obama alimkumbatia Rais Kikwete akimwelezea kama “kaka wa karibu na rafiki mzuri” kauli na kitendo ambacho kiliwashangaza mamia ya watu waliokuwa kwenye ukumbi.
JK: TUWASAIDIE WACONGO, WAMECHOSHWA NA VITA
RAIS KIKWETE |
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameitaka
Jumuia ya Kimataifa kufanya kila linalowezekana kumaliza mzozo wa kisiasa na
mapigano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ili kutoa nafasi kwa wananchi wa Congo kuishi katika amani
na kujitafutia maendeleo.
“Hawa
ni watu walioteseka sana na kwa muda mrefu, wana haki ya kupata amani, wana
haki ya kupata muda wa kupumzika kutokana na vita na mapigano,” Rais
Kikwete ameuambia mkutano wa pili wa wakuu wa nchi zilizotia saini mkataba wa
kutafuta amani, usalama na ushirikiano katika DRC chini ya Umoja wa Mataifa (UN).
Katika
mkutano huo, uliofanyika leo, Jumatatu, Septemba 23, 2013, kwenye Umoja wa
Mataifa mjini New York chini ya Uenyekiti wa Katibu Mkuu wa UN, Mheshimiwa Ban Ki Moon kama
ulivyokuwa mkutano wa kwanza uliofanyika Februari 24, mwaka huu, 2013, mjini
Addis Ababa, Ethiopia, Rais Kikwete amewaambia viongozi wenzake wa nchi
wanachama wa Umoja wa Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR)
na wengine waliotia saini mkataba huo:
“Nadhani
hatua zilizochukuliwa mpaka sasa kuhusu DRC ni nzuri na mchakato wa kutafuta
amani nchini humo unakwenda vizuri. Ni muhimu tukafikia mwisho wa tatizo hili
kwa sababu wananchi wa DRC wametesema mno na kwa muda mrefu. Wana haki ya
kupata amani, wana haki ya kupata muda wa kutosha wa kufanya mambo ya maana
kama ya maendeleo yao badala ya kukaa na kufikiria vita,”
Rais Kikwete amesema kwenye mkutano huo.
Rais
Kikwete amesema kuwa siri ya kufanikiwa katika DRC ni kutekeleza yale yote
ambayo nchi hizo zimekubaliana kutekeleza katika DRC akisisitiza: “La
msingi ni kila mmoja wetu kutekeleza yale yote tuliyokubaliana. Hiyo ndiyo siri
ya kuleta amani na utulivu katika DRC.”
Mbali
na Rais Kikwete, mkutano huo wa leo umehudhuriwa na Rais Yoweri Museveni wa
Uganda ambaye pia ni Mwenyekiti wa ICGLR,
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Rais Joseph Kabila Kabange wa DRC, Rais Paul Kagame wa Rwanda, Rais
Joyce Banda wa Malawi ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa
Afrika (SADC), Mwenyekiti wa
Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU)
Mheshimiwa Nkosazana Dlamini-Zuma, na Katibu Mkuu wa UN ambaye alikuwa mwenyekiti wa mkutano huo.
Aidha,
mkutano huo umehudhuriwa na Makamu wa Rais na wawakilishi wa Jamhuri ya Congo
(Congo-Brazzaville), Zambia, Angola na Sudan Kusini.
Kwenye
mkutano huo, wasemaji wengi wamesisitiza kuwa hakuna amani ya kweli katika DRC
na nchi za Maziwa Wakuu bila viongozi wa nchi hizo kukubali kuzungumza na
kukubaliana na vikundi mbali mbali ambavyo vinapigana dhidi ya baadhi ya nchi
hizo.
Baadaye
leo, Rais Kikwete amehudhuria mkutano wa Baraza la Uongozi la Umoja wa Kutafuta
Usalama wa Chakula na Ushirikiano wa Grow
Africa uliofanyika kwenye Ofisi za Taasisi ya Uchumi Duniani (WEF)
uliofanyika kwenye ofisi za taasisi hiyo katika Marekani mjini New York.
Rais
alizungumza kwa ufupi katika mkutano huo ambako alitaka wafadhili wa miradi ya
kilimo katika Afrika kuongeza kasi ya kutoa fedha za kuleta mageuzi ya kilimo
katika Bara la Afrika kwa sababu kila mmoja wa wadau anatekeleza majukumu yake
kwa haraka zaidi kuliko wafadhili.
MZEE MWINYI AWAONYA WANAOTUMIA ELIMU NA UJUZI WAO KUANGAMIZA USTAWI WA JAMII
Elizabeth Mwase Programu Manager wa Mtandao wa
Watoto na Vijana kutoka Imani Mbalimbali (GNRC) akimpokea Mzee Ali
Hassan Mwinyi Rais Mstaafu wa awamu ya pili ambaye alikuwa mgeni rasmi
ya Siku ya Kimataifa ya Amani iliyoadhimishwa mwishoni mwa Juma jijini
Dar es Salaam ukumbi wa Don Bosco.
Mgeni Rasmi Mzee Mwinyi akisalimiana na baadhi ya
mabalozi na wawakilishi wa jumuiya za maendeleo za nchi wa hisani
wakati wa maadhimisho hayo jijini Dar es Salaam.
Mgeni Rasmi Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaji
Ali Hassan Mwinyi akipokea mfano wa ndege wa Amani kutoka kwa
wanafunzi wa shule mbalimbali za jijini Dar es Salaam wakati wa
maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Amani duniani jijini
Dar.
Mgeni Rasmi Mzee Mwinyi akihutubia wageni waalikwa
(Hawapo pichani) wakati wa sherehe za Siku ya Kimataifa ya Amani leo
asubuhi jijini Dar. Kulia ni balozi wa Rwanda nchini Ben Rugangazi na
kushoto kwa mgeni rasmi ni Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa
la kuhudumia Watoto (UNICEF) Jama Gulaid.
Meza kuu.
Baadhi ya wanafunzi wa sekondari mbalimbali za
jijini wakitumbuiza kwa nyimbo mbalimbali zenye ujumbe wa kudumisha
Amani na upendo duniani.
Mgeni Rasmi Mzee Mwinyi akiwa katika picha ya
pamoja na baadhi ya mabalozi na wawakilishi wa ofisi za mabalozi
waliohudhuria sherehe hizo kwenye ukumbi wa Don
Bosco.
Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria sherehe
hizo.
MZEE MWINYI AWAONYA WANAOTUMIA ELIMU NA UJUZI WAO KUANGAMIZA USTAWI WA JAMII
*Awaasa vijana kutotumiwa na wanasiasa kwa maslahi
yao
*Ashangaa wajuzi walivyompachika jina la Ruksa enzi
za miaka 1990s
Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Alhaji Ali Hassan
Mwinyi amesema kuna baadhi ya watu katika jamii hutumia elimu, ujuzi
na maarifa yao kuangamiza, kubomoa na kudumaza Ustawi wa Jamii kwa
maslahi binafsi na si ya Umma. Mo blog inaripoti.
Mzee mwinyi amesema hayo wakati wa kuadhimisha siku
ya Kimataifa ya Amani Duniani inayoadhimishwa 21th Septemba kila mwaka
ambayo imefanyika katika ukumbi wa Don Bosco jijini Dar es Salaam,
amesema kuna baadhi ya watu wanatumia elimu yao vibaya kwa kupanga
kuua watu wengine kwa maslahi yao aidha ya kisiasa au ya
kiuchumi.
“Elimu kwa kawaida kuleta matokeo mazuri kwa jamii
husika endapo itatumika sawia kwa malengo yaliyokusudiwa na kwa
maendeleo endelevu ya taifa kwa ujumla, ila kuna baadhi ya wanajamii
kutumia ujuzi huu vibaya na kuangamiza ustawi wa jamii husika,”
amesema.
Mzee Mwinyi aliendelea kusema kwamba katika
kuadhimisha siku ya kimataifa ya amani duniani yenye kauli mbiu
“Education for Peace” ni lazima elimu kwa ajili ya amani iwe endelevu
hapa duniani ili iweze kuleta suluhu na utengamano katika jamii na
mataifa yote duniani.
Amesema kwamba vijana nchini lazima waepuke kutumiwa
na wanasiasa kwa maslahi yao ya kisiasa na wajifunze kutatua matatizo
yao kwa njia ya amani bila ya kuwa na mihemko, jazba, misongo na
hasira ili kuendelea kudumisha amani na upendo katika nchi yetu ambayo
ni kisiwa cha amani.
“nawaasa vijana wakitanzania wa leo hata kama
mmenyimwa haki zenu ni bora kutumia njia ya kistaarabu na kutumia
elimu mnayopata mashuleni bila kusahau macho, masikio na vipawa vyenu
mlivyopewa na mwenyezi mungu katika kutafuta haki yenu kwa njia ya
amani bila misukosuko,” aliongeza.
Mzee Mwinyi alitumia nafasi hiyo kuwashangaa baadhi
ya watu kwa kutumia ujuzi na elimu yao kwa kumpachika jina la Ruksa
bila yeye kujua wametumia muktha gani kumpa jina hilo, lakini Mzee
Mwinyi alitumia jukwaa hilo pia kuwapa ruksa vijana kutumia elimu yao
kuleta hali ya amani na utulivu ndani ya nchi.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa
Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) Jama Gulaid amesema kwamba Umoja
wa Mataifa uliweka maazimio siku ya kimataifa ya amani duniani ili
watu wanaogombana na kupigana kwa shida mbalimbali kupata nafasi ya
kuweka silaha zao chini katika siku hii adhimu.
Amesema kupitia azimio hilo ambalo lilizinduliwa
mwaka 1982 kwa mara kwanza linatambua uwepo wa watu wanaoathirika na
vita katika sehemu mbalimbali duniani na waliokwishapoteza maisha
kutokana na matatizo vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Naye Mratibu na Mtathimini wa Mtandao wa watoto na
vijana kutoka Imani Mbalimbali (GNRC) Bi, Joyce Mdachi amesema swala
la amani na utulivu linaanzia kwenye kaya hadi ngazi ya taifa kwahiyo
ni muhimu kwa jamii na vijana kuelewa amani inaanzia
nyumbani.
“jamii iliyolelewa katika mazingira mazuri ina nafasi
kubwa ya kuleta matokeo chanya kwenye mustakabali wa taifa kwa ujumla
lakini jamii iliyolelewa vibaya haiwezi kubadilisha taifa kwa sababu
ni zao la tunda baya,” alisema.
Mdachi alisisitiza kwamba kuporomoka kwa maadili
ndani ya jamii ya leo swala hilo pia lilianzia kwenye kaya ya mtu
mmoja mmoja hadi ngazi ya taifa ambapo leo hii taifa linashuhudia
mambo ya kifisadi, rushwa na ubadhilifu wa mali za umma kunakofanywa
na viongozi waandamizi.
ATHUMANI HAMIS BALOZI WA USALAMA BARABARANI KWA UTHAMINI WA AIRTEL
Mkurugenzi
wa Mawasiliano wa Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi
Airtel (T) ambao wamekuwa wadhamini wakuu wa Maadhimisho ya wiki
ya Nenda kwa Usalama Barabarani kwa mwaka wa tano mfululizo Bi.
Beatrice Singano Mallya akisalimiana na Mwandishi wa Habari Athumani
Hamisi ambaye ameteuliwa kuwa balozi wa Usalama Barabarani na
kudhaminiwa na Airtel katika wiki hii ya usalama barabarani mkoani
mwanza. Athumani alipata ajali ya gari ambayo ilisababisha baadhi ya
viungo vyake kupooza licha ya kupata matibabu nchini Afrika ya Kusini
na India.
MWANZA, TANZANIA
KAMPUNI ya Mawasiliano ya Simu ya Airtel imesema kuwa itahakikisha suala la Usalama barabarani linazingatiwa na jamii ya Watanzania ili kupunguza ajali za barabarani .
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Mallya kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Usalama Barabarani,yanayofanyika Jijini Mwanza.
Alisema kama wadau wa usalama barabarani,wamedhamini maadhimisho hayo ili kuwezesha jamii kupata elimu na uelewa kuhusu matumizi ya barabara,sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani katika kupunguza ajali nchini.
Alisema ajali nyingi nchini zinachelewesha maendeleo na kupunguza uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.
“Sisi kama wadau tumedhamini maadhimisho haya kwa mwaka wa tano mfululizo,lengo letu tunataka jamii ipate uelewa na hatimaye kupunguza ajali za barabarani zinaoweza kuepukika,ndiyo sababu tuko hapa,” alisema.
Alisema kutokana na kuonesha umahiri wameanzisha mfumo mpya wa ulipiaji wa leseni za magari kwa kupitia njia ya Airtel Money.
------
1. usalama barabarani airtel 1
Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Emmanuel Nchimbi akisalimiana na
Mwandishi wa Habari Athumani Hamisi ambaye ameteuliwa kuwa balozi wa Usalama Barabarani na kudhaminiwa na Airtel katika wiki ya usalama barabarani, mwandishi huyu alipata ajali ya gari ambayo ilisababisha baadhi ya viungo vyake kupooza licha ya kupata matibabu nchini Afrika ya Kusini na India.
1. usalama barabarani airtel 2 na 3
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi
Airtel Tanzania ambao wamekuwa wadhamini wakuu wa Maadhimisho ya wiki
ya Nenda kwa Usalama Barabarani kwa mwaka wa tano mfululizo Bi.
Beatrice Singano Mallya akisalimiana na Mwandishi wa Habari Athumani
Hamisi ambaye ameteuliwa kuwa balozi wa Usalama Barabarani na
kudhaminiwa na Airtel katika wiki hii ya usalama barabarani mkoani
mwanza. Athumani alipata ajali ya gari ambayo ilisababisha baadhi ya
viungo vyake kupooza licha ya kupata matibabu nchini Afrika ya Kusini
na India.
MWANZA, TANZANIA
KAMPUNI ya Mawasiliano ya Simu ya Airtel imesema kuwa itahakikisha suala la Usalama barabarani linazingatiwa na jamii ya Watanzania ili kupunguza ajali za barabarani .
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Mallya kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Usalama Barabarani,yanayofanyika Jijini Mwanza.
Alisema kama wadau wa usalama barabarani,wamedhamini maadhimisho hayo ili kuwezesha jamii kupata elimu na uelewa kuhusu matumizi ya barabara,sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani katika kupunguza ajali nchini.
Alisema ajali nyingi nchini zinachelewesha maendeleo na kupunguza uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.
“Sisi kama wadau tumedhamini maadhimisho haya kwa mwaka wa tano mfululizo,lengo letu tunataka jamii ipate uelewa na hatimaye kupunguza ajali za barabarani zinaoweza kuepukika,ndiyo sababu tuko hapa,” alisema.
Alisema kutokana na kuonesha umahiri wameanzisha mfumo mpya wa ulipiaji wa leseni za magari kwa kupitia njia ya Airtel Money.
------
1. usalama barabarani airtel 1
Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Emmanuel Nchimbi akisalimiana na
Mwandishi wa Habari Athumani Hamisi ambaye ameteuliwa kuwa balozi wa Usalama Barabarani na kudhaminiwa na Airtel katika wiki ya usalama barabarani, mwandishi huyu alipata ajali ya gari ambayo ilisababisha baadhi ya viungo vyake kupooza licha ya kupata matibabu nchini Afrika ya Kusini na India.
1. usalama barabarani airtel 2 na 3
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi
Airtel Tanzania ambao wamekuwa wadhamini wakuu wa Maadhimisho ya wiki
ya Nenda kwa Usalama Barabarani kwa mwaka wa tano mfululizo Bi.
Beatrice Singano Mallya akisalimiana na Mwandishi wa Habari Athumani
Hamisi ambaye ameteuliwa kuwa balozi wa Usalama Barabarani na
kudhaminiwa na Airtel katika wiki hii ya usalama barabarani mkoani
mwanza. Athumani alipata ajali ya gari ambayo ilisababisha baadhi ya
viungo vyake kupooza licha ya kupata matibabu nchini Afrika ya Kusini
na India.
WANAOTUMIA TAKWIMU ZA UONGO KUKIONA:SERIKALI
Sep 23, 2013
DAR ES SALAAM, Tanzania
KAMISHNA wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012, Hajjat Amina
Mrisho ametoa onyo kwa watu watakaotumia takwimu ambazo si sahihi wakati
wanapotoa taarifa mbalimbali kuwa wawe makini kwa kuwa sheria ya kuwabana iko mbioni.
Aidha Hajjat Amina amesema
kwamba kwa watendaji wa Serikali, na
wanasiasa watakaotoa takwimu za uongo
katika taarifa mbalimbali wajiandae kuong’ooka
katika nyadhifa zao.
Kauli hiyo
imetolewa leo na Kamshina huyo wakati
akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya
Taifa ya Takwimu(NBS) kuhusu uzinduzi wa kitabu cha pili cha idadi ya watu cha umri na jinsi, ambacho
kitasaidia kupanga mikakati mbalimbali ya kimaendeleo.
“Muswada wa Sheria
ya Takwimu wa mwaka 2013 imeshasomwa mara ya
kwanza Bungeni ,unasubiriwa kusomwa kwa
mara ya pili katika Bunge lijalo. Hivyo itakapokamilika sisi tutapambana na watu wanaotoa takwimu
ambazo si sahihi. Kwa watendaji wa Serikali watakaotumia takwimu ambazo si
sahihi wakati wanapotoa taarifa mbalimbali mfano tatizo la njaa linawakabili
watu kiwango kipi wajiandae kufukuzwa kazi,” alisema Hajjat Amina.
Alisema suala linatakiwa pia kuzingatiwa watu
wataotangaza au kuandika,wakiwemo waandishi wa habari takwimu zilizotajwa na mtu bila ya kufanyiwa
uchunguzi kupitia mtandao wa ofisi hiyo watachukuliwa hatua kulingana na sheria
hiyo.
Hajjat Amina
alifafanua kuwa takwimu hizo zitakuwa zitaboreshwa kwa kila mwaka, hivyo aliwataka
watu kuzitumia ipasavyo kulingana na
taarifa za kila mwaka.
Akizungunzia
kuhusu uzinduzi huo, alisema utafanyika Septemba 25, mwaka huu katika ukumbi wa
mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere uliopo jijini Dares Salaam, ambapo mgeni
rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Sief Ali
Iddi .
POLISI WATATU WAFARIKI, NANE WAJERUHIWA KATIKA AJALI YA GARI WAKITOKA KATIKA OPERESHENI KIMBUNGA
Na Chibura Makorongo,Kahama
POLISI watutu wa wa mkoa wa Njombe wamekufa na wengine
wanane kujeruhiwa wakiwemo maofisa uhamiaji baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka
katika kijiji cha Malenge wilayani
Kahama mkoa wa Shinyanga.
Ajali hiyi imetokea ikihusisha gari lenye namba PT 0762 aina ya Landrover 110 kupinduka
jana saa 12:00 jioni lilipokuwa likitokea mkoani Kagera katika
operesheni Kimbunga ya kuwaondoa wahamiaji haramu ambapo lilikuwa njiani kurudi mkoani Njombe.
Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Kihenye Kihenya
alisema marehemu hao walitambulika kwa
jina moja kuwa ni PC Marco wa kituo cha polisi Njombe, D-CPL Fredy pamoja na PC Sufiani wote wa kituo cha polisi
Makambako.
Aidha kaimu kamanda aliwataja majeruhi ambao ni askari
polisi kuwa ni Pc Hussein aliyepata jeraha kichwani pamoja na mguu wa kushoto
na hali yake inalezwa kuwa ni mbaya ambapo hadi sasa hajazinduka, Inspekta Leornad aliyemia kiuno, PC Yusuph
ambaye ndiye dereva wa gari hilo aliyeumia kiuno wote kutoka kituo cha Njombe.
Wengine ni DC Lambuli
aliyeumia paji la uso pamoja na mguu wa kulia, PC James aliyeumia goti pamoja
na mkono wa kushoto pamoja na PC Adamu aliyeumia paji la uso nao kutoka kituo
cha polisi cha Njombe.
Maafisa uhamiaji waliokuwemo kwenye ajli hiyo aliwataja kuwa
ni Glory Temu kutoka mkoa wa Mbeya na inaelezwa kuwa hali yake ni mbaya ambapo
hadi sasa hajapata fahamu pamoja na Augustino Nanyambe kutoka mkoa wa Rukwa
aliyeumia goti pamoja na mkono wa kushoto.
Kamanda Kihenya alisema kuwa miili ya marehemu hao imehifadhiwa
katika hospitali ya wilaya ya Kahama huku pia majeruhi hao wakipatiwa matibabu
katika hospitali hiyo na kuongeza kuwa chanzo cha ajali hiyo hakijafahamika
ambapo polisi bado wanaendelea na uchunguzi.
CCM YAWA LULU NYAMONGO, WILAYANI TARIME
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kama ishara ya kufungua ofisi ya CCM Tawi la Nyabichune,wilaya ya Tarime mkoani Mara.
Ofisi ya CCM Tawi la Nyabichune wilaya ya Tarime mkoani Mara ambalo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alilizindua rasmi leo tarehe 23 Septemba 2013..
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Nyamongo na kuwaeleza namna ambavyo wamejipanga kutatua tatizo la muda mrefu baina ya wakazi wa eneo hilo na wamiliki wa mgodi wa North Mara .
Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza mmoja wa wakazi wa Nyamongo Chacha Magayo Butora ambaye alifafanua kwa kina matatizo yanayowakabili wakazi wa eneo hilo,Katibu Mkuu alitumia Demokrasia ya hali ya juu baada ya kuwapa nafasi watu watatu mbali mbali ambao wananchi waliwachagua waje kuelezea matatizo yao.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Nyamongo wilaya ya Tarime mkoani mara ambapo aliamua kufuta kila kitu kwenye ratiba yake na kutaka wananchi wateue wawakilishi wao ili wakakae kikao na watu wa serikali ili kupata ufumbuzi wa matatizo hayo.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini Ndugu Stephen Masele akifafanua mambo kadhaa ambayo Wizara yake inataka wananchi wafaidike na migodi ikiwa pamoja na kuwasaidia wachimbaji wadogowadogo ambao wanatakiwa wajiunge kutengeneza vikundi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wakiongea na wananchi wa Nyamongo ,Wananchi wa Nyamongo wameshukuru sana kwa kusikilizwa kwa ukaribu haijawahi tokea na wameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Viongozi hao.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisoma moja ya taarifa inayofafanua matatizo ya wakazi wa Nyamongo.
Baadhi ya wakazi wa Nyamongo wakiwa kwenye kikao cha ndani pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana,Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye,Naibu Waziri Nishati na Madini Ndugu Stephen Masele na Viongozi wengine wa Serikali ambapo walikaa na kujadili matatizo yao namna ya kuyatatua.
No comments:
Post a Comment