EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Tuesday, July 16, 2013

WAKATI MATIKEO YA UCHAGUZI ARUSHA YAKIZUA MAKUBWA, MNYIKA AMTAKA ATOA TAMKO ZITO DHIDI YA RAIS KIKWETE

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), amemtaka Rais Jakaya Kikwete, kujitokeza hadharani na kukiri kuwa Ikulu imeshindwa kusimamia kauli aliyoitoa juu ya ujenzi wa kituo kipya cha mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi (UBT).
Pia Mnyika amemtaka Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi ajitokeze ndani ya wiki moja na aeleze sababu ya kumdanganya Rais Kikwete kuwa kituo kipya cha mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi kingekamilika Januari mwaka huu.
Mnyika alitoa kauli hiyo jana alipofanya ziara ya kushtukiza katika kituo cha mabasi Ubungo kwa ajili ya kujionea miundombinu ya kituo hicho baada ya kufanyika ubomoaji wa awali na kusitishwa kwa huduma muhimu ndani ya kituo hicho.
“Kama rais alitoa agizo na halikusimamiwa, anapaswa arudi na atuambie kuwa ameshindwa kusimamia kauli yake, lakini pia Meya Masaburi aseme hadharani kuwa walimuongopea rais juu ya upatikanaji wa kituo kabla ya Januari mwaka huu, kwa kuwa sasa ni miezi sita imepita na hakuna taarifa yoyote wala maandalizi ya kuwapo kwa kituo hicho,” alisema Mnyika.
Katika ziara hiyo Mnyika alishuhudia adha wanazopata abiria ikiwamo ukosefu wa vyoo vya uhakika, eneo la kujihifadhi wakati wa mvua pamoja na kukosekana kwa gereji ndani ya kituo hicho.
Aidha, abiria walimueleza mbunge huyo namna wanavvyolipa kiingilio katika mageti ya kuingilia ndani huku kukiwa hakuna huduma yoyote wanayopata wakiwa ndani.
Kwa upande wao wafanyakazi wa kada tofauti ndani ya kituo hicho walielezea kero wanazokabiliana nazo baada ya kituo hicho kuvunjwa.
Kwa upande wa madereva walieleza kuwa licha ya Sumatra kuagiza wamiliki wa mabasi ya abiria kuwapatia mikataba ya ajira madereva wao suala hilo halijafanyika mpaka sasa.

Ushindi wa CHADEMA waibua mazito

  WAKATI ushindi wa kishindo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jijini Arusha ukimweka pabaya Meya wa Jiji la Arusha, mazito mengine yameibuka baada ya Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Sipora Liana, kutoboa siri kubwa.

Mbele ya madiwani wapya wa CHADEMA wakiongozwa na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Liana alisema alikuwa anafikiria ‘kukimbia’ kutokana na hali tete ya usalama kugubika jiji hili.
Katika kikao kifupi cha utambulisho wa madiwani hao wapya, Liana alisema: “Wakati ninakuja hapa (Arusha) kulikuwa na taarifa za vurugu na maandamano, jambo ambalo lilinifanya nifikirie kama hali ingeendelea kuwa hivyo  nitaomba niondoke, lakini nimeridhishwa na utulivu uliokuwepo  jana (juzi),” alisema Mkurugenzi Liana.
Kauli hiyo ilimfanya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, kumweleza mkurugenzi huyo kuwa hata wao CHADEMA wataendelea kumpa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha kuna kuwapo maendeleo ya wananchi wa jiji hilo, hasa kutokana na namna alivyoonyesha ushirikiano wakati wa uchaguzi huo.
Alisema kuwa halmashauri hiyo inakabiliwa na kashfa za ufisadi wa mabilioni ya fedha za wananchi, jambo alilosema kuwa madiwani na wabunge wa CHADEMA wako tayari kumsaidia kuyafumua yote ili wayashughulikie  kwa masilahi ya wananchi wa Arusha na si vyama vya siasa.
“Kwa namna ulivyotoa ushirikiano (siku ya uchaguzi) kila nilipokupigia simu hata kwa suala dogo ulikuwa unahakikisha linapatiwa ufumbuzi hata zile taarifa kuwa uliletwa kuhakikisha CHADEMA haichukui hata kiti kimoja cha udiwani sasa imeondoka,” alisema Lema.
Lema alisema kuwa nao wameanza kupata imani na mkurugenzi huyo kwa namna alivyoendesha uchaguzi huo, kwani awali waliambiwa kuwa aliletwa kwa ajili ya kuhakikisha CHADEMA hairudishi kata hizo.
Mkurugenzi huyo alimjibu Lema kuwa yeye yupo kwenye jiji hilo kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wote bila kujali itikadi za vyama, huku akiwaahidi ushirikiano madiwani hao ambapo alisema kuwa atahakikisha fedha za wananchi zinalindwa, huku akisisitiza kuwa jambo hilo anaweza kulifanya  hata bila madiwani, kwani hata  madiwani hao nao wakienda kinyume huwa anawakamata.
“Diwani aliyechaguliwa na wananchi ndiye nitakayefanya naye kazi, ila na yeye akileta masuala binafsi, hapo na mimi atanikuta,” alisema Liana, jambo lililofanya watu wote kucheka.
Naye Katibu wa CHADEMA Kanda ya Arusha, Amani Golugwa, alimpongeza mkurugenzi huyo kwa namna alivyosimamia uchaguzi huo na kumtaka aendelee hivyo hivyo ili ile dhana kuwa CHADEMA ndio wanasababisha vurugu Arusha iondoke na ukweli ujulikane kuwa wanaosababisha vurugu mara zote ni watawala.
Madiwani hao wapya na kata zao kwenye mabano, Bryson Ngowi (Kimandolu), Emanuel Kessy (Kaloleni), Millace Kinabo (Themi) na Jeremiah Mpinga (Elerai), ambao walisindikizwa na msafara mkubwa wa viongozi na mashabiki  wa CHADEMA ulioanzia kwenye ofisi zao za Mkoa wa Arusha zilizoko Ngarenaro na kupita kwenye Barabara ya Sokoine kuelekea kwenye ofisi hizo za mkurugenzi, hali iliyoamsha shamrashara kwa wananchi kila walipokuwa wakipita.
Msafara huo uliojumuisha magari, pikipiki na waenda kwa miguu, ambapo madiwani hao pamoja na Lema walikuwa kwenye gari la wazi, hali iliyosababisha  shughuli kusimama kwa muda kila ulipokuwa ukipita, huku kelele za zamu ya meya kung’oka zikivuma kila mahali.

No comments:

Post a Comment