Kampuni ya Apple
watengenezaji wa simu aina ya iPhone imesema itafanya uchunguzi juu ya
madai ya mwanamke mmoja wa China aliyedaiwa kupoteza maisha kwa kupigwa
shoti wakati akizungumza kwa simu yake ya iPhone aliyokuwa anaicharge.
Madai
hayo yamewasilishwa na msichana kutoka magharibi mwa China Xinjiang,
aliyeandika barua kwa mtandao maarufu wa China ‘Sina Weibo’ kuelezea
kilichomsibu dada yake mkubwa Ma Ailun aliyekuwa na miaka 23.
Kwa
mujibu wa taarifa hiyo, polisi wamethibitisha kifo cha msichana huyo
kimetokana na shoti ya umeme, lakini haijathibitishwa bado kama simu
yake ilihusika.
Msemaji wa Apple nchini China Carolyn Wu amesema
wanafanya uchunguzi juu ya tukio hilo na pia akatoa pole kwa familia ya
marehemu. “We will fully investigate and cooperate with authorities in
this matter,” Alisema.
No comments:
Post a Comment