EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, April 10, 2014

MASTAA MAN UNITED WALICHOBAKIZA MSIMU HUU NI KUHAKIKISHA HAWATIMULIWI!

DARREN_FLETCHER-16JAN14KIUNGO wa Manchester United, Darren Fletcher, amekiri kuwa kilichobakia kwao Msimu huu kama Wachezaji ni kucheza vizuri Mechi zilizobaki ili kujihakikishia wanabakishwa kwenye Timu ambayo inatarajiwa kujengwa upya.
Jumatano Usiku, Man United ilichapwa Bao 3-1 na Bayern Munich kwenye Robo Fainali ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, na kutupwa nje kwa Jumla ya Bao 4-2 katika Mechi mbili.
Matokeo hayo yanamaanisha Msimu wa Mabingwa hao wa England sasa umekwisha.
Yapo matumaini madogo mno kwamba wanaweza kuliua pengo la Pointi 7 kati yao na Timu iliyo nafasi ya 4 kwenye Ligi Kuu England huku wakiwa wamebakiza Mechi 5 ili wao wacheze UCL Msimu ujao.
Kwa mujibu wa Darren Fletcher, ambae aliongea mara baada ya kufungwa huko Munich, kilichobaki ni kwa Wachezaji hao hao walioiangusha Timu Msimu huu kujituma katika Mechi zilizobaki ili wabakie kwenye Kikosi kipya Msimu ujao.
Jana, Meneja wa Timu, David Moyes, alidokeza kuwa mwishoni mwa Msimu wataijenga upya Timu na wapo Wachezaji ambao washawasuka ili kuhamia Old Trafford.
Uamuzi huu unamaanisha kuwa wapo Wachezaji kadhaa itabidi wauzwe ili wapya waje.
Fletcher amefafanua: “Wachezaji ni lazima wacheze vizuri ili wabaki kwenye mipango ya Meneja. Ipo minong’ono mingi kuwa yatakuwepo mabadiliko makubwa!”

Wachambuzi wamedai Moyes atalazimika kusaini Wachezaji kadhaa wapya wakiwemo, Sentahafu, Mafulbeki wawili na Viungo wawili ili kuimarisha Timu na kuanza kuijenga upya.
Akigusia uwezekano wa kukosa kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI kwa mara ya kwanza tangu Mwaka 1995, Fletcher alisema: “Hatutafikiria hilo, tutafikiria kutwaa Ubingwa na kurudi Ulaya kama Mabingwa!”
Kuhusu uwezekano wa wao kucheza EUROPA LIGI Msimu ujao, Fletcher alisema: “Tuikumbatie! Twende na kutwaa Kombe!”

No comments:

Post a Comment