![]() |
MKUU WA MKOA WA LINDI KATIKATI.. |
Vyama vya ushirika vya kuuza na kununua mazao wilaya
ya Nachingwea mkoani Lindi, vimechangia zaidi ya sh.milioni 62 kwa ajili ya ujenzi
wa maabara ya shule ya sekondari ya wasichana wilayani humo.
Hayo yameelezwa na Afisa Ushirika wa wilaya ya
Nachingwea Lameck Chota wakati alipokuwa akitoa taarifa ya ujenzi wa maabara
hiyo, kwa mkuu wa mkoa wa Lindi Ludovick Mwananzila alipokuwa kwenye ziara siku
tatu ya kukagua miradi ya maendeleo wilaya.
Chota amesema uongozi wa halmashauri hiyo kupitia
idara ya ushirika iliviomba vya vya msingi kutenga shs 10 kwa kila kilo moja ya
ufuta na korosho iliyouzwa katika vyama hivyo, ili kuchangia mradi wa ujenzi wa
maabara ya shule ya sekondari ya wasichana Nachingwea.
![]() | |||||||||||
WANAFUNZI NA VIONGOZI MBALIMBALI WAKISHUHUDIA UJENZI WA JENGO LA SHULE (darasa) |
Afisa Ushirika huyo amesema awamu ya kwanza ya msimu
wa 2012/13 vyama vya ushirika nane kati ya 23, vilichangia ujumla ya shs
milioni 42 ambazo zilisaidia kuanza mchakato wa kuanzisha ujenzi wa maabara
hiyo.
Amesema ili ujenzi wa maabara hiyo uweze kukamilika
zaidi ya shs milioni 39 zinahitaji, ambazo zinatarajiwa kuchangwa na vyama
ambavyo havijachanga hadi sasa, na kuongeza kuwa wilaya hiyo ina vyama 23 na
hadi sasa vyama 13 tu vimewasilisha michango yake.
Chanzo, Mwanja Ibadi.LINDI
No comments:
Post a Comment