EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, February 26, 2014

SUMATRA YATOA MAFUNZO YA SHERIA ZA BARABARANI KWA SHULE MBALIMBALI MKOANI MTWARA



Wakuu wa shule, Waalimu na viongozi mbalimbali nchini, wametakiwa kushirikiana na serikali pamoja na taasisi zilizokasimiwa na mamlaka ya kusimamia uendeshaji wa huduma ya usafiri wa majini na nchi kavu (SUMATRA), ili kuhakikisha kuwa elimu ya haki na wajibu inafika kwa usahihi kwa walengwa wa utumiaji wa huduma hiyo.

Wito huu umetolewa na Afisa Elimu Mkoa wa Mtwara HIPSON KIPENYA, wakati wa hotuba yake ya kuzindua vyama vya wanafunzi mashuleni vya watumiaji wa huduma ya usafiri wa nchi kavu na majini katika mkoa huo.

Amesema kuwa kwa kutoa elimu ya haki na wajibu kwa mtumiaji wa vyombo vya usafirishaji, kutasaidia vyombo hivyo kutoa huduma kwa mujibu wa matakwa ya sheria, na mikataba baina ya watumiaji na mtoa huduma ya usafiri.



Kipenya amewataka walimu wakuu wa shule, wakurugenzi wa halmashauri, kwa kushirikiana na Baraza la SUMATRA mkoa, kufuata sheria na taratibu zilizopo za ufundishaji katika sekta ya elimu, kwa kuwapa nafasi wanafunzi kujifunza na kushiriki matukio pale inapobidi.

Afisa Elimu huyo ameitaka kamati na Baraza kuwa makini, kuweka mikakati na mbinu madhubuti za kuwaelimisha wananchi kufahamu haki na wajibu wao na kupata mwitikio wa watumiaji wengi wa huduma za usafiri wa majini na nchi kavu.



Chanzo, SUMATRA, Mary Mpandula – Pride fm.

No comments:

Post a Comment