EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Monday, February 24, 2014

MKUU WA WILAYA MTWARA AGEUKIA CCM UUZAJI WA ARDHI



VIONGOZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika halmashauri ya Mtwara Vijijini, wametakiwa kuwa makini na viongozi wa serikali za vijijini wanaojihusisha na uuzaji ardhi kiholela, ili kudhibiti upungufu wa ardhi siku za usoni, kunakotokana na ardhi kupungua huku vizazi vikiongezeka.
Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Mtwara, Williman Kapenjama Ndille wakati akiwasilisha Utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa miaka miwili ya kuanzia January hadi Disemba 2012 na January hadi Disemba mwaka 2013, katika mkutano wa halmashauri kuu ya CCM Mtwara vijijini na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Benjamini Mkapa uliopo katika chuo cha ualimu Mtwara Kawaida.
Amewakumbusha viongozi hao wa chama kuwa, wajibu wao mkubwa ni kutoa elimu kwa wananchi juu ya faida za kuhifadhi ardhi kwa manufaa yao ya sasa na vizazi vinavyokuja, ili kuja kuiwekeza kwa faida kwa siku za baadae.
Akizungumzia sekta ya kilimo amesema kuwa mwaka huu hali ya chakula hairidhishi, kutokana na upungufu wa mvua, na wakati mwingine kunyesha kwa kiwango cha juu hali inayochangia kuharibu mazao yaliyo mashambani.
Awali akizungumza katika mkutano huo wa halmashauri kuu ya CCM Mtwara Vijijini, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mtwara Mohammed Sinani amesisitiza kuwa ni wajibu wa viongozi wa chama kuwajengea wananchi mazingira ya kuondokana na umasikini, kwa kuhakikisha wanawaelekeza kwa wataalamu walio katika halmashauri mkoani humo.
Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo amewaonya wale wote wenye nia ya kutangaza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ikiwemo ubunge na udiwani kuwa muda huo bado, na amewataka kuwaacha wali madarakani kumaliza vipindi vyao vya uongozi, huku akiwataka viongozi wote kulipigia kelele suala hilo, ili kuepuka siasa za makundi, kubaguana na kupakana matope.
                                         Chanzo, CCM.

No comments:

Post a Comment