Reporters/ Mohamedi & Aloyce
Wafanyakazi wa makampuni mbalimbali ya ulinzi Mkoani
Mtwara wameuomba uongozi wa makampuni hayo kuwaongezea mishahara na kulipwa
malipo yao kwa wakati.
Hayo yamezungumzwa mapema hii leo na baadhi ya
wafanyakazi hao wakati walipokuwa wanazungumza na waandishi wa habari wa Prde
Fm Radio.
Wafanyakazi hao ambao hawakupenda majina yao yatajwe
wamesema kuwa hawalipwi malipo yao kwa wakati na vilevile kuwepo kwa vitendo
vya unyanyasaji hali inayopelekea maisha yao kuwa magumu.
Pia wafanyakazi hao wameuomba uongozi wa makampuni
hayo kushughulikia matatizo yao likiwemo la kutopewa likizo ilikuepukana na
matatizo ambayo wamekuwa wakiyapata.
No comments:
Post a Comment