EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Friday, January 31, 2014

MAJUNGU,WIVU VYAMNG'OA STONE VIJANA JAZZ



Na Mshamu Ngojwike,
Msanii Wa Zamani Wa Bendi Ya Vijana Jazz,Kida Waziri “Stone Lady” Amesema Majungu,Wivu Na Ubinafsi Vilimfanya Ang’atuke Kwenye Kundi Hilo Ambalo Lilikuwa Maarufu Miaka Ya 80.
Kida Ambaye Amerudi Tena Kwenye Mziki Wa Dansi Akiwa Kama “Solo Artists” Huku Ataimba Nyimbo Za Zamani Ambazo Ameimba Wakati Yupo Vijana Jazz.
Akizungumza Kwa Hisia Kali, Kwenye Jukwaa La Sanaa Ambalo Linafanyika Kila Jumatatu Katika Ukumbi Wa Baraza La Sanaa Tanzania(Basata) Alisema  Pamoja Na Kupotea Kwa Muda Mrefu Vitu Ambavyo Vilimfanya Akae Pembeni Na Mziki Kutokana Majungu,Wivu Na Ubinafsi Ambavyo Alikutana Nazo Kila Kukicha.

“Kipindi Kile Kwa Kweli Nilikuwa Kipindi Kigumu Sana,Wanamziki Wenzangu Walikuwa Wananifanyia Visa Kila Kukicha Hadi Kupelekea Niachane Kabisa Na Mziki Ambao Zaidi Ya Miaka 20 Nilkuwa Kando Na Tasnia Hii” Alisema.
Waziri Alisema Awezi Kusahau Aliposhushwa Jukwaani, Na Viongozi Wa Wajuu Wa Vijana Jazz,Ambapo Akikumbuka Upelekea Kumwaga Machozi.
Alisema Kwa Sasa Yupo Kwenye Maandalizi Ya Mwisho Ya Kuandaa Albamu Ambayo Itahusisha Na Nyimbo Ambazo Aliziimba Zamani  Akiwa Vijana Jazz Akiwa Na Marehemu Baba Watoto Wake,Hemedi Maneti Ambazo Ameziongezea Ubora Kama “Penzi Haligawanyiki” Sehemu Ya 1&2 Na “Mawifi Mnaninyanayasa” .

No comments:

Post a Comment