EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Friday, January 31, 2014

CCM YASHUKIWA UPOTEVU WA CHOPA YA CHADEMA WADAI WAMEPANGA NJAMA KUWAANGUSHA. Wakati NCHEMBA ASEMA CHADEMA ISIWATISHE WANANCHI




HELIKOPTA ya Chadema maarufu kama Chopa, juzi ilipotea angani na kusababisha viongozi wa chama hicho kushindwa kufanya mkutano katika Kijiji cha Mpwayungu wilayani Chamwino, kama ilivyokuwa imepangwa kwenye ratiba.
Kwa mujibu wa ratiba iliyokuwa imepangwa, viongozi wa kitaifa ambao ni Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (BAVICHA), walikuwa wafanye mkutano katika kijiji hicho saa 4 asubuhi.
Akizungumza na MTANZANIA, Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Dodoma, Steven Massawe alikiri kupotea kwa helikopta hiyo na kukanusha kwamba hakuna njama zozote zilizofanywa na CCM kutokana na kupotea kwa helikopta hiyo.
Kijiji cha Mpwayungu kipo katika Kata ya Mpwayungu, ambayo nafasi ya udiwani ipo wazi na vyama vya Chadema na CCM vyote vimesimamisha wagombea.
“Sababu kubwa ya kupotea kwa helikopta ni tatizo la mawasiliano kama mnavyojua Kijiji cha Mpwayungu hakina mawasiliano. Helikopta ilikuwa ifike katika Kijiji cha Mpwayungu saa nne asubuhi, lakini Kapteni alipotea na kusababisha kukaa angani kwa saa moja na dakika arobaini na akatua Kijiji cha Chipogolo.
“Alipofika Chipogolo akaambiwa sio kijiji hicho chenye mkutano na akatakiwa kurudi nyuma kwa upande wa magharibi kwa kilometa 40, hata hivyo hakufanikiwa ikabidi arudi mjini kujaza mafuta,” alisema Massawe.
Alisema baada ya kujaza mafuta, viongozi hao hawakwenda tena kufanya mkutano Mpwayungu badala yake wakaenda Mpwapwa ambapo kulikuwa na mkutano mwingine saa 7 mchana kwa mujibu wa ratiba.
“Leo (jana) hii viongozi hao kwa kutumia helikopta wamekwenda tena Mpwayungu na kufanikiwa kufanya mkutano majira ya saa nne asubuni na baada ya hapo waliekea Kijiji cha Segala Wilaya ya Chamwino, baadaye wataenda Kiteto na Moshi,” alisema.
Alisema sio kweli kwamba CCM walifanya njama helikopta ya Chadema ipotee ili isifanye mkutano katika kijiji hicho na kwamba Chadema na CCM vyote vilishafanya uzinduzi wa kapteni katika kata hiyo.
“Chadema ilifanya uzinduzi wake wa kampeni katika Kata ya Mwayungu, Januari 26 mwaka huu na CCM walifanya uzinduzi wao Januari 20,” alisema Massawe.
Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, amesema iwapo Serikali ya CCM haitaweka mazingira ya haki kwa makundi mbalimbali ndani ya jamii kwa ajili ya amani ya kudumu, migogoro ya ardhi italitumbukiza taifa katika sintofahamu na hatari kubwa nchini.
Dk. Slaa aliyasema hayo kwenye mikutano ya M4C Pamoja Daima, jana alipokuwa akiwahutubia wananchi wa maeneo ya Iselamagazi, Kishapu, Mhunze, Itilima, Lugulu na Bariadi.
Alisema ni haki kwa wananchi kuwa na matumaini, kwani ndiyo misingi wa amani ya kweli ambayo haihitaji kuhubiriwa jukwaani.
Chama cha mapinduzi (CCM) kimesema kuwa kinashangazwa na kitendo cha chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema)kutumia Helikpota kwenye chaguzi zake huku kikidai kuwa ni mkombozi wa wananchi jambo ambalo ni kujitafutia sifa na umaarufu pekee kwa wananchi.
Hayo yameelezwa na Naibu Katibu mkuu wa CCM ambaye pia ni Naibu waziri wa fedha Mwigulu Nchemba wakati akifungua rasmi kampeni za udiwani katika kata ya Sombetini . Mwigulu alisema kuwa CCM inashangaa sana Chadema kutumia Helikpota kwenye chaguzi nyingi hapa nchini jambo ambalo wanaonesha wazi kuwa wanatumia gharama kubwa kwa ajili ya kuongeza sifa kwani gharama ambazo zinatumika hadi kumalizika kwa kampeni ni zaidi ya Milioni 200.
Alisema kuwa Gharama ambayo inatumika kwenye uendeshaji wa Helkopta ni gharama ambayo ingeweza kuwasaidia wanachama wao. “Wananchi wa kata ya Sombetini napenda kuwaambia kuwa hata sisi wenyewe huwa tunashangaa sana ujio wa hii Helikopta na ninapenda kusema wazi helikopta hiyo inakuja ili iweze kuwazubaisha ninyi, sasa msikubali kudanganywa na helikopta bali angalieni sera za mgombea “aliongeza Mwigulu


Pia aliwataka wananchi kuhakikisha kuwa kamwe hawatumiki kwenye siasa za sifa na ushahbiki kwani siasa hizo wakati mwingine zinasababisha hata vifo vya watu ambao hawana hatia ya kufa ovyo: “wananchi mnapswa kujua na kutambua kuwa siasa za sasa zimebadilika sana msikubali kuwa mashabiki wa siasa bali mnatakiwa kuangalia zaidi sera za vyama na mahitaji yenu msije mkachagua kiongozi kwa ushabiki itawagharimu sana kwenye utendaji”aliongeza Mwigulu
Awali Mgombea Udiwani katika kata hiyo ya Sombetini kwa tiketi ya CCM Bw David Mollel alisema kuwa ana mikakati mingi sana ya kuhakikisha kuwa anasaidia kata hiyo endapo atapata ridhaa ya kuongoza rasmi kama diwani .David alisema kuwa changamoto ambazo atahakikisha kuwa anazitatua ni pamoja na urekebishaji wa barabara, uboreshaji wa masoko,kna uimarishaji wa vikundi vya wanawake na jamii kwa ujumla

No comments:

Post a Comment