EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Friday, January 31, 2014

Justin Bieber ajipeleka kizimbani mwenyewe



TORONTO, Canada

MWANAMUZIKI,  Justin Bieber  amefunguliwa mashitaka ya shambulizi dhidi ya dereva wa teksi  alilofanya mwezi mmoja uliopita mjini  Toronto nchini Canada.

Habari kutoka nchini humo zilieleza jana kuwa, Bieber aliwasili Kituo cha Polisi mjini  Toronto na kulakiwa na umati wa wapiga picha, waandishi wa habari na mashabiki hali ambayo iliwalazimu polisi wa kituoni hapo kulazimika kutengeneza njia ili kumsindikiza,  Bieber aweze kupita mlangoni na kuingia ndani ya kituoni hicho.

Kwa mujibu wa taarifa za Polisi,  tukio hilo lilitokea baada ya dereva wa gari hilo kupeleka kundi la watu sita kwenye klabu moja ya usiku mjini Toronto muda wa saa 9 alfajiri Desemba 30 mwaka  jana.


"Wakati dereva akiwapeleka watu hao sita  hotelini  yalitokea mabishano kati ya dereva na mmoja wa abiria," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo ya polisi.. "Baada ya mabishano hayo  abiria mmoja alimpiga nyuma ya kichwa mara kadhaa dereva  hali ambayo ilimlazimisha  kusimamisha gari na kuita polisi,”iliongeza sehemu ya taarifa hiyo.
Taarifa za kituo cha televisheni cha CTV, Bieber aliondoka kwenye kituo cha polisi mjini  Toronto   usiku wa kuamkia jana na polisi wanasema kwamba anatarajia kurejea kituoni hapo Machi 10 mwaka huu.


 

No comments:

Post a Comment