EBENEZA MARCH 9 2014
SWACO
royal
tt
NIMO
mvuto
Wednesday, October 9, 2013
MZOZO WA BAJETI UNAVYOMCHANGANYA RAIS OBAMA
NEW YORK
Rais Barack Obama wa Marekani amewaalika wabunge wa baraza la wawakilishi kutoka chama chake cha Democratic, kukutana nae leo ili kujadili mzozo wa bajeti na hali inayokaribia ya muda wa mwisho wa kulipa madeni.
Afisa wa Ikulu ya Marekani amesema kuwa huu utakuwa mwanzo wa mazungumzo kadhaa anayotarajia kuyafanya na wabunge wa vyama vyote.Afisa huyo amesema kuwa makundi mengine ya wabunge , ikiwa ni pamoja na wale wa Republican kutoka mabaraza yote ya bunge la Marekani, yaani Congress, wataalikwa katika siku zinazokuja.
Ikiwa hakuonekani kupatikana suluhisho hivi karibuni katika mzozo huo wa bajeti ulioanza kuyumbisha masoko ya hisa , mkutano huo unaashiria mwanzo wa juhudi za kuepusha hatua ya kushindwa kulipa madeni, ambapo imebakia wiki moja kabla ya muda wa mwisho kumalizika.Obama ameonya kuwa kutatokea mparaganyiko na matatizo makubwa ya kiuchumi iwapo taifa hilo litaruhusiwa kufikia hatua ya kushindwa kulipa madeni yake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment