![]() |
| waandamanaji misri wakiwa wamebeba picha ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Muhamad Muls |
Rais Mohammed Mursi aliyeondolewa madarakani nchini Misri, atafikishwa mahakamani Novemba 4 kwa madai ya kuchochea mauaji ya wapinzani wake wakati akiwa madarakani.
Mahakama ya Misri imesema leo kuwa Mursi pamoja na wanachama wengine 14 wa chama chake cha Udugu wa Kiislamu, watafikishwa mahakamani , ikiwa ni pamoja na wasaidizi wa ngazi ya juu na wanachama waaandamizi wa kundi hilo.
![]() |
| misri wakati wa machafuko |
Mursi aliondolewa madarakani katika mapinduzi Julai 3 mwaka huu, na amekuwa akishikiliwa mahali pasipojulikana na hajaonekana tangu wakati huo, licha ya kuwa amezungumza na familia yake mara mbili, na alitembelewa na mkuu wa sera za mambo ya kigeni wa Umoja wa ulaya Catherine Ashton , pamoja na ujumbe wa Umoja wa Afrika.
Mahakama hiyo ya rufaa ya mjini Cairo imemtaja jaji Ahmed Sabry Youseff kuendesha kesi hiyo.


No comments:
Post a Comment