EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, October 9, 2013

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI YA MADAI YA KAMPUNI ZA SIMU ZA MKONONI NCHINI


MAHAKAMANI

NA:FARAJI MAARUFU
Mahakama kuu kanda ya Dar es salaam imetupilia mbali pingamizi lililokua limewekwa na upande wa serikali, la kupinga makampuni matano ya simu kuunganisha madai yao dhidi ya serikali, kupinga kuwepo kwa tozo ya shilingi elfu moja katika laini za simu.
Kesi iliyopo mbele ya jopo la majaji watatu ikiongozwa na jaji Aloyce Mujunguzi, imefunguliwa na chama cha kutetea walaji nchini ambacho kinapinga kukatwa kwa kodi hiyo.
Akitoa maelezo hayo kiongozi wa jopo hilo jaji  Mujunguzi, amesema kuwa mahakama imeona kuwa upande wa serikali hauna hoja za msingi, hivyo anaziruhusu kampuni hizo kuungana na chama cha walaji kupinga tozo hiyo.Katika shauri hilo chama hicho pamoja na kampuni za simu za Airtel, Zantel, Ttcl, Vodacom na tigo, zinatetewa na mawakili wanaoongozwa na wakili Fatma Karume, wakati upande wa serikali unaongozwa na wakili Aloycea Mbuya.
Shauri hilo limepewa muda na jaji hadi tarehe kumi na tano mwezi huu, ili kampuni hizo ziwe zimewasilisha mambo ambayo wanataka yafanyiwe kazi, ili yaunganishwe na mambo yaliyokwisha wasilishwa na chama cha walaji.
Jaji huyo pia ameutaka upande wa serikali, hadi itakapofika tarehe 21 ya mwezi huu uwe umejibu maelezo ambayo yatakua yameelezwa na upande wa pili wa walalamikaji, na baada ya hapo mahakama itaanza kushughulikia kesi hiyo.

No comments:

Post a Comment