EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, October 9, 2013

KIDATO CHA PILI WAELEZEA MTIHANI WAO



MTWARA-
NA:kassim Ngumbi
Watahiniwa wa kidato cha pili katika shule ya sekondari ya Aman Islamic iliyoko katika Manispaa ya Mtwara Mikindani, wameishukuru serikali kwa kurudisha mitihani ya kidato cha pili mashuleni.
Hayo yamesemwa na mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo Juma Yussuf alipokuwa akizungumza na mwandishi wa pride fm radio shuleni hapo mapema hii leo, ambapo amesema kuwa kurudishwa kwa mitihani ya kidato cha pili mashuleni, kutasaidia wanafunzi kujijengea mazoea ya kujisomea mara kwa mara kwa lengo la kufanya mitihani hiyo.
Amesema kuwa mitihani hiyo ya kidato cha pili itaongeza umakini kwa wanafunzi katika kufuatilia masomo yao, na itasaidia kuwa na wanafunzi wenye kujiamini na kujitambua kuwa wao ni wanafunzi, kwani mara nyingi ukuaji wa vijana huanzia kipindi ambacho wapo mashuleni.
Pia Juma amesema kuwa, wanashukuru kutokana na maswali mengi yanayotungwa katika mitihani hiyo yanaendana na masomo ambayo tayari yamekwishafundishwa, huku pia upande wa usimamizi ukiwa wa kawaida, ambapo wanatarajia kumaliza mitihani hiyo Ijumaa ya Oktoba 11 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment