KIUNGO mahiri wa klabu
ya Manchester United, Darren Fletcher amevaa jezi ya klabu hiyo kwa mara
ya kwanza katika kipindi cha miezi 10 iliyopita baada ya kupoana
vidonda vya tumbo vilivyokuwa vikimsumbua.
Fletcher
ambaye alikosa mechi nyingi msimu uliopita baada ya kufanyiwa upasuaji
wa kuondoa vidonda vya tumbo vilivyokuwa ikimsumbua alicheza dakika 67
katika mchezo wa vijana wa chini ya umri wa miaka 21 dhidi ya Fulham
ambapo timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.
Fletcher
alianza mazoezi rasmi katikati ya Septemba na muda si mrefu anaweza
kurejea katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo kama hali yake
ikiimarika. Katika
mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa AJ Bell uliopo Salford
ulishuhudiwa na wengine wa zamani wa United kama David Beckham, Phil
Neville na Nicky Butt
No comments:
Post a Comment