EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, October 30, 2013

MESSI, RIBERY, RONALDO WAONGOZA ORODHA YA BALLON D'OR.


  
majembe katika kinyang'anyilo mwana soka bora ulaya
SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limetoa orodha ya wachezaji 23 watakaogombea tuzo ya mchezaji bora wa dunia maarufu kama Ballon d’Or. Miongoni mwa wachezaji waliopo katika orodha hizo ni pamoja na Lionel Messi ambaye anashikilia taji hilo aliloshinda mwaka jana, Franck Ribery wa Bayern Munich na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid. Bayern ambao ni mabingwa wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya msimu uliopita ndio waliotoa wachezaji wengi zaidi katika orodha hiyo ambapo mbali na Ribery pia wapo Philipp Lahm, Thomas Muller, Manuel Neuer, Arjen Robben na Bastian Schweinsteiger. Mapema Mwezi Desemba mwaka huu FIFA na France Football watatangaza orodha ya majina matatu watakaopata kura nyingi zaidi kabla ya mshindi wa tuzo hiyo kutangazwa katika hafla itakayofanyika jijini Zurich, Januari 13 mwakani.

No comments:

Post a Comment