EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, November 6, 2013

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE KULIHUTUBIA BUNGE KESHO



Rais Jakaya Mrisho Kikwete, kesho mchana anatarajiwa kulihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kutokana na ratiba hiyo Serikali imewaelekeza Mawaziri na Manaibu Waziri kutotoka nje ya Dodoma hadi hapo Rais atakapokuwa amehutubia Bunge. 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania
Aidha  safari zote za Kamati za Bunge ambazo zilikuwa katika mchakato wa kutekelezwa zimeahirishwa hadi baada ya kesho, ili kutoa fursa kwa wabunge wote kuwapo wakati wa hotuba hiyo.
Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah amethibitisha jana katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma, kuwapo kwa ratiba ya Rais Kikwete kesho Alhamisi kulihutubia Bunge. Rais Kikwete atalihutubia Bunge wakati likisubiri kujadili mapendekezo ya marekebisho katika Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya 2013, ambayo ilipitishwa katika mkutano uliopita.

No comments:

Post a Comment