GENEVA.
Benki ya Dunia imetoa mkopo wa dola milioni 340 kwa
nchi tatu za Kiafrika za Tanzania, Burundi na Rwanda, zitakazotumika kwa ujenzi
wa bwawa la kuzalisha umeme katika eneo la Rusumo.
Taarifa zinasema kuwa, bwawa hilo la kuzalisha umeme
litakamilika mwaka 2020, ambalo litakuwa na uwezo wa kuzalisha megawati 80 za
umeme.
Mawaziri wa Fedha wa nchi za Tanzania, Burundi na
Rwanda wametia saini makubaliano ya utekelezwaji wa mradi huo, ambao
unadhaminiwa na Benki ya Dunia.Mradi huo utasaidia kuongeza nguvu za umeme katika
nchi hizo tatu, ambazo ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Wadadisi wa masuala ya kisiasa wanasema kuwa, ujenzi
wa bwawa hilo la umeme kwa kiasi kikubwa utaziba ufa ambao ulianza kujitokeza
kwenye uhusiano wa Tanzania na Rwanda katika miezi ya hivi karibuni.


No comments:
Post a Comment