EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Monday, October 14, 2013

KIFO CHA ARAFAT WA PARESTINA NI UTATA MTUPU

Ofisa wa Palestina amesema hakuna taarifa mpya zilizotolewa kuhusu chanzo cha kifo cha aliyekuwa mwenyekiti wa mamlaka ya utawala wa Palestina Yasser Arafat. 
 Tawfi Al Tirawi, mkuu wa kamati iliyokuwa inachunguza chanzo cha kifo cha Arafat amesema habari zilizotolewa na jarida moja la Uingereza zinazosema kifo cha Arafat kilitokana na sumu, si habari mpya kwani habari hizo zinatokana na ripoti iliyoandaliwa na televisheni ya Al Jazeera.
Amesema hadi sasa wanaendelea kusubiri taarifa rasmi kutoka kwa wachunguzi.Kutokana na ripoti ya televisheni ya Al Jazeera iliyosema kifo cha Arafat kilitokana na sumu aina ya polonium 210, na nguo zake ziligunduliwa kuwa na sumu hiyo.Kutokana na habari hizo mwezi Novemba mwaka jana wataalamu wa Ufaransa, Uswisi na Urusi walifukua mwili wa Arafat na kuchukua sampuli kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

No comments:

Post a Comment